Home » »

Mtoto anadaiwa kuwa ni Nabii, anawatuhumu watu kuwa wachawi.

HEKAHEKA-2013 

Hii inatoka Mbezi Dar, kwenye Hekaheka ya leo msichana anayeishi na wazazi wake akapata ujauzito lakini alipojifungua akajifungua chatu baadaye chatu huyo akabadilika na kuwa binadamu wa kawaida.
Mama mmoja anatuhumiwa kuwa mchawi, amesema alipata taarifa kuwa mtoto huyo ambaye kwa sasa wanamuita nabii alipandisha mashetani na kumtaja mama huyo kwamba ni mchawi, huwa anamchukua na kumpeleka makaburini, baada ya tuhuma nyingi kuenea kuhusu yeye kuna siku watu walitaka kumuua, akaona aende Kanisani kumuelezea Paroko juu ya matukio hayo.
Mama mmoja muuza samaki amesema kuwa mtoto huyo nabii alimtuhumu kuwa mchawi na kuwaambia watu kuwa biashara za samaki na dagaa anazofanya sio samaki ila ni sehemu za siri za watoto wadogo, kitu kilichofanya biashara yake kuwa ngumu.
Kijana mmoja amesema watu hao ni matapeli wanaokosanisha watu na huyo mtoto ambaye wanadai ni nabii aliyezaliwa chatu sio kweli ingawa walimuona msichana huyo wakati akiwa mjamzito, waliwahi kutoa taarifa katika Ofisi za Serikali za mtaa wakakaa kikao lakini muafaka haukupatikana.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog