List ya wachezaji ambao Man City iko mbioni kuwaondoa kwenye kikosi cha timu hiyo.
Kipigo cha Manchester City dhidi ya Barcelona cha bao 1-0 huenda kimekuwa moja ya sababu ya kocha mkuu wa timu hiyo Manuel Pellegrini kuamua kuwaondoa katika orodha yake baadhi ya wachezaji wa kikosi chake akiwemo Yaya Toure.
Mabingwa hao wa ligi ya Uingereza wamepanga kuwauza baadhi ya nyota wake msimu huu akiwemo Yaya Toure, Gale Clichy, Pablo Zabaleta, Jesus Navas, Fernandinho, Steven Jovetic na Edin Dzeko.
Man City ilishindwa kutinga hatua ya robo fainali dhidi ya Barcelona katika
mechi ya kombe la klabu bingwa Ulaya na kocha wake amethibitisha kwamba
mabadiliko makubwa yatafanyika ndani ya klabu hiyo.
0 comments:
Post a Comment