Home » »

CHADEMA YAHITIMISHA KURA ZA MAONI UCHAGUZI MDOGO JIMBO LA KALENGA, MWANASHERIA MWENDA AIBUKA KIDEDEA

[Image]
Sinkala Mwenda akiwa amenyanyuliwa juu baada ya ushindi wa kura za maoni juzi
MGOMBEA Sinkala Mwenda ameibuka kidedea wa kura za maoni za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika mchakato wa kumpata mgombea atakayepeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Kalenga.
Kura hizo za maoni zilizofanyika juzi katika ukumbi wa St Dominic, mjini hapa zilishirikisha wagombea 13.
Jimbo la Kalenga liko wazi baada ya aliyekuwa mbunge wake, Dk William Mgimwa kufariki dunia Januari 1, mwaka huu.
Mwenda mwanasheia aliyemaliza shahada yake ya sheria katika chuo cha Ruaha Iringa, aliibuka kidedea baada ya kupata kura 132 dhidi ya kura 122 alizopata mshindani wake wa mkuu Grace Tendega.
Kabla ya kura hizo kuanza kupigwa wajumbe wengi walisikika wakimpigia chapuo, Tendega wakidai ana historia nzuri ya kisiasa katika jimbo hilo kwa kuzingatia kwamba katika Uchaguzi Mkuu wa 2010 aligombea ubunge katika hilo kupitia chama cha Jahazi Asilia na kutoa upinzani mkubwa kwa Dk Mgimwa.
Mwingine aliyekuwa akipewa nafasi ni Zuberi Mwachula ambaye hata hivyo kutokuwepo kwake katika kura hizo za maoni kulisababisha wajumbe wamuadhibu kwa kutompa kura hata moja.
Pamoja na kurudisha fomu za kuomba kuteuliwa na chama hicho, Mwachula aliyekuwa Meneja wa Shirika la Kimataifa la Concern mkoa wa Iringa alishindwa kuhudhuria katika mchakato huo kwa kile kilichoelezwa kwamba yuko nje ya nchi kikazi.
Naye kijana machachari ambaye ni wakala na muuza magazeti maarufu mjini Iringa, Aidan Pungili pamoja na kumudu jukwaa kutokana na uwezo wake wa kujieleza vizuri aliambulia kura 2.
Uchaguzi  huo uliomalizika majira ya saa 4 usiku jana ulisimamiwa na Mjumbe  wa Kamati  Kuu ya Chadema Taifa Chiku  Abwao  na Mkurugunzi wa Oparesheni na Mafunzo ya chama hicho Benson  Kigaila.
Wagombea  wengine ambao  wameonyesha  kufanya vema kiasi  baada ya  kujiunga na Chadema  wakitokea  CCM ni pamoja na Dr Evaristo Mtitu  aliyepata  kura 32 na Ancent Sambala kura 22.
Wengine walioshiriki kura hizo na kura zao kwenye mabano ni  Akbar Sanga (21), Rehema Makoga (4), Henry Kavina (9), Mussa Mdede (48), Mchungaji Samweli  Nyakunga (2) na Mwalimu Vitus Lawa akipata kura (14).
Katika nasaha zake kwa wagombea na wajumbe, Kigaila alisema ushindi wa kura za maoni sio kigezo pekee kinachotumiwa na Chadema kupata mgombea.
“Tunataka hili lieleweke, huu ni mwanzo wa mchakato. Ni lazima tupate mgombea kwa kuzingatia mazingira ya Kalenga, awe anakubali ndani ya chama na kwa wapiga kura wajimbo hilo kwasababu tunataka kushinda,” alisema.
Alisema baada ya kura hizo za maoni Kamati Kuu ya Chadema Taifa itakutana kesho Ijumaa, Februari 14 na kufanya maamuzi ya mwisho kwa kuzingatia mambo mengi zikiwemo taarifa za kiintelejensia za ndani ya chama.
“Tuna heshimu sana kura za maoni, lakini sio kigezo pekee. Watanzania wana imani sana na Chadema, kitakachotufanya tushinde ni aina ya mgombea tunayempeleka kwa watu, vinginevyo tunaweza kufanya kampeni kubwa na tukashindwa,” alisema.

Taarifa za awali kutoka ndani ya chama hicho zimedai kwamba katika kampeni zao watatumia helkopta mbili na magari nane ya chama  ili kuyafikia makundi ya wapiga kura kwa kasi zaidi.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog