Home » »

BREAKING NEWSSssssss CCM WASHINDA KWA KISHINDO KATA ZOTE TATU MKOA WA IRINGA , NJOMBE CHADEMA WAIGALAGAZA CCM .........................................................

CHAMA  cha  mapinduzi (CCM)  mkoa  wa  Iringa  kimefanikiwa  kutetea kata  zake  zote tatu ambazo  leo   wananchi  wameshiriki  kupiga kura  kuwachagua madiwani  kufuatia nafasi hiyo kuwa wazi baada ya madiwani wake kufariki  dunia  huku chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) kikishindwa  vibaya katika  uchaguzi huo.

Mbunge  wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa (Chadema) ambae  alikuwepo  eneo la Nduli  akifuatilia  matokeo  ya uchaguzi huo pamoja na  wafuasi wa Chadema  alilazimika  kuondoka katika eneo hilo  baada ya  kubaini kuwa hali ya ushindi kwa Chadema ni ndoto.
Huku   wafuasia  wa  CCM  wakionekana  kumpongeza  aliyekuwa mgombea wa CCM kata ya Nduli pamoja na  kaimu katibu wa CCM mkoa wa Iringa  Hassan Mtenga kuwa  kazi  yake imeonyesha inaonyesha  wazi  safari yake ya  kulitwaa jimbo la Iringa mjini .

Katika  Matokeo hayo ambayo hadi sasa  majira ya saa 12.50  bado msimamizi wa uchaguzi kutangaza CCM inaongoza kwa kura 810 huku  Chadema  wakifuatia kwa kura 491

Mbali ya  matokeo  hayo ya kata ya  Nduli pia  CCM imeshinda kata ya Ibumi na Ukumbi zote za  wilaya ya  Kilolo.

Wakati katika kata ya  Njombe mjini mgombea  wa  Chadema amepata  kukibwaga vibaya  chama  cha Mapinduzi (CCM) ambapo  matokeo yanaonyesha  mgombea wa CCM amepata  kuongoza kituo kimoja pekee   kwa tofauti ya  kura  2  huku  vituo vyote  Chadema ikiibuka kidedea.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog