Home » »

Nyota Ya Lowassa Bado Inang'aa: Utafiti Mpya Waonyesha Anaongoza Kwa Kupendwa na Wapiga Kura Wengi......Wafuatia Slaa, Magufuli na Membe


Nyota ya Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa, imeendelea kung’aa baada ya Taasisi ya Samunge Social Sciences Research Center (SSSRC), kufanya utafiti na kubaini kuwa kiongozi huyo ni chaguo la kwanza kwa wananchi.

Utafiti huo uliofanywa miaka miwili kuanzia 2013 hadi 2015, unaonyesha Lowassa anaongoza kwa asilimia 20.7 dhidi  ya wagombea 31.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mtafiti Mkuu wa SSSRC, George Nyaronga, alisema utafiti huo waliufanya kwa kutumia madodoso pamoja na mahojiano kwenye mikoa 18.

Utafiti huo na asilimia walizopata wanasiasa wengine kwenye mabano ni Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema, Dk. Willbrod Slaa asilimia 11.7; Waziri wa Ujenzi, John Magufuli (7.6); Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (7); Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba (4.8); Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba (4.2)  na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe 3.4 sawa na Kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda (2.4) na Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi, James Mbatia (1.2).

Alisema pia utafiti huo ulionyesha kuwa Lowassa pekee ndiye anayekubalika na wapiga kura wengi, karibia idadi sawa ya jinsia zote mbili, wanaume 50 na wanawake 49.

Kwa ujumla, Lowassa na vinara wengine 10 wanaotajwa kuwania urais walipata asilimia 67.2, huku asilimia zilizobaki (32.8) zikitwaliwa na wagombea wengine 10 kati ya 20 waliohusishwa katika utafiti huo.

Aidha, Nyaronga alisema hawakuwa na dodoso  linaloorodhesha majina ya wanaopendekezwa kuwa Rais ila majina yalitajwa na wajaza madodoso wenyewe kisha wao wakajaza majina kwenye SSSRC.

Kwa mujibu wa dodoso lenye kichwa cha habari cha katika tafiti kuhusu uchaguzi wa mwaka 2015, takwimu zinaonyesha kuwa Watanzania wanamtaka mtu mwenye kufanya maamuzi magumu.

Alisema kwa maoni ya wengi waliohojiwa na kujaza dodoso, wanaonyesha kuwa Lowassa anakubalika zaidi na kwamba ulifanywa katika mikoa 18 ya Bara na Visiwani, watu 1,000 walijaza dodoso na 6,000 walifanyawa mahojiano.

Alisema utafiti huo uliofanywa kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Zanzibar, Morogoro, Singida, Shinyanga, Mwanza, Mara, Mbeya, Katavi, Kigoma, Tabora, Arusha, Moshi, Iringa, Njombe, Songea, Lindi na Mtwara .

Nyaronga alisema baadhi ya mambo ambayo tafiti hiyo ilikuwa ikitafuta majibu ni masuala yanayohusu changamoto kwa Tanzania kwa sasa, sifa za kiongozi anayehitajika kukabiliana na changamoto hizo, mapendekezo ya jina la Rais atakayesimamia vizuri changamoto hizo, chama chenye uwezo wa kutupatia rais ajaye kwa mujibu wa katiba ya mwaka 1977 na kama Watanzania watapiga kura.

Vyama  vya  Siasa
Alisema utafiti huo umebaini CCM ina asilimia 53.5 ya kutoa Rais , Chadema yenye asilimia 34.2.

Alisema  vijana wa miaka kati ya 18-25 ambao ni sawa na asilimia 46 wanamtaka Lowassa kuwa Rais, ikifuatiwa na vijana wa miaka 26-30, na  vijana wa kati ya miaka 30-35.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog