Home » »

              


Huyu Ndo Zitto Kabwe Ninayemfahamu Ambaye CHADEMA Wameamua Kumpaka Matope.


Sijawahi  kuwa  Mwanachama  wa  Chama  cha  ACT-Wazalendo  na sijafikiria  kujiunga  na  chama  hicho. Nilishawahi  kuwa  Mwanachama  mtiifu  wa  chama  cha  Demokrasia  na  maendeleo (Chadema)

Nikiwa  ndani  ya CHADEMA  nimewahi  shiriki  katika  harakati  nyingi  zote  zikiwa  na  lengo  la  kukikuza  chama  ambacho  niliamini  ndo  mkombozi  wa  kweli  wa  mtanzania.

Bahati  mbaya  sikuwa  sahihi, nilikosea  kukiamini  chama  hicho  ambacho  idadi  kubwa  ya  viongozi  wake  ni  mahafidhina.

Nikiwa  ndani  ya  siasa, nimefanikiwa  kujuana  na  wanasiasa  wengi  wakubwa  kwa  wadogo, mmoja  wao  ni  kiongozi  mkuu  wa  ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe.

Namjua  Zitto, nafahamiana  naye  vizuri, ni  mmoja  wa  wanasiasa  wasomi, wenye  siasa  safi  ambaye  mara  zote  kauli na  hoja  zake  zimetaliwa na  busara  na  nia  ya  kulijenga  taifa, siwezi  kusema  si  mbinafsi  moja  kwa  moja  lakini  nina  imani  nae  kubwa  kuwa  si  mbinafsi.

Zitto  ameweza  kuzimudu  siasa  safi  za  taka  zilizokuwa  zikiendeshwa  ndani  na  nje  ya  chadema  kabla  ya  kuhamia  ACT- Wazalendo.Ameweza  kupambana  na  kupenya  kwenye  changamoto  nyingi  za  kisiasa  hasa  siasa  hizi  za  kuwa  na  chama  kimoja  kikongwe  na  chenye  nguvu  nchini  na  nje  ya  nchi.

Sote  tunaijua  CCM  ni  chama  chenye  wanachama  na  viongozi  wanaoijua  siasa, wanaweza  kukibadili  chama  hicho  wakati  wowote, chama  hiki  kikuu  nchini  ni  kama  kinyonga, kinabadiilika  kulingana  na  mazingira  na  wakati.

CCM  kinapanga  vyema  karata  zake, kina  propaganda  zenye  kuwiana  na  ukweli  tofauti  na  ilivyo  kwa  upinzani  ambao  wanadanganya  wananchi  mpaka  wanajidanganya  wao  wenyewe.

Zitto  ameweza  kupenya  kote  huku  na  ndio  maana  leo  hii,  Zitto  anaposulubiwa  hata  CCM  kinaumia  na  kumhurumia, kwa  sababu  wanamjua  mwanasiasa  huyu  kijana  ni  mtu  wa  namna  gani.

Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog