HII KALI..!! BINTI AMUUA MAMA YAKE MZAZI BAADA YA KUMLAZIMISHA KUFUA NGUO CHAFU
Si jambo la kawaida
kusikia mtoto kamuua mama yake ama mama kamuua mtoto wake, japo kwa
miaka ya sasa matukio kama hayo yameshamiri kwa kiasi kikubwa sehemu
mbalimbali duniani.
Tukio la mtoto kumuua mama yake leo limechukua headlines huko Zimbabwe baada ya kutokea kutoelewana baina yao.
Kilichotokea ni kwamba
binti wa miaka 17 amemuua mama yake kwa kumchoma moto baada kulazimishwa
kufua nguo chafu, kitendo kilichomkasirisha na kufikia uamuzi huo.
Kabla ya kumuua mama yake kwa kumwagia mafuta kisha kumchoma moto, mama
yake alimpiga kitendo kilichomuuzi binti huyo na kufanya uamuzi huo
mgumu.
Polisi wamemfungulia mtoto huyo mashtaka ya mauaji licha ya kupewa taarifa kuwa alikua akisumbuliwa na ugonjwa wa akili.
0 comments:
Post a Comment