Home » » DEREVA BODABODA IRINGA ATEKWA NA KUUAWA NA WATU WASIOJULIKANA

DEREVA BODABODA IRINGA ATEKWA NA KUUAWA NA WATU WASIOJULIKANA

           
  IRINGA
Zikiwa  zimepita  siku  chache  toka  mmoja kati ya madereva boda boda mjini Iringa kutekwa kisha  kujeruhiwa vibaya kablaya kuporwa  pikipiki  yake ,unyama huo dhidi ya madereva  boda boda  umeendelea kutikisa mji wa Iringa baada Kijana mmoja mkazi wa kihodombi kutekwa kisha kuuwawa kinyama.


Tukio hilo la kinyama  limetokea  usiku  wa  leo baada ya kijana  huyo aliyetambulika kwa  jina la Edger Lalika kukutwa ameuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani .

Mashuhuda  wa  tukio hilo    wamesema  kuwa tukio la kuuwawa  kwa  dereva  boda  boda  huyo liletokea eneo la  Tosamaganga wilaya ya Iringa mkoani Iringa.

Hata  hivyo kijana  huyo anayekadiliwa  kuwa na umri wa miaka 25,ameuwa akiwa anafanya shughuli zake za bodaboda baada  ya  kukodiwa na mteja  wake huyo ambae aliamua  kuitoa roho yake kabla ya kumpokonya boda boda.

Kutokana na tukio  hilo  baadhi ya madereva bodaboda wamelaani vikali kitendo hicho na kuwataka madereva bodaboda wengine kuungana na kushirikiana na jeshi la polisi kufichua vitendo hivyo  vya utekaji na mauwaji  dhidi ya madereva  boda boda.
 

akithibitisha kutokea kwa tukio hilo  kamanda wa jeshi la polisi mkoani iringa bw ramadhan mungi amelaani vikali kutokea kwa mauaji hayo na kuiomba jamii kutoa ushirikiano wa kutosha ili kumbaini mhusika
 
    

Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog