Home » » NIWAKATI WA KUOMBA DUNIA SASA IMEHARIBIKA

NIWAKATI WA KUOMBA DUNIA SASA IMEHARIBIKA

HIVI NDIVYO MWANANCHI WA KIJIJI CHA WENDA ALIVYOCHUNWA NGOZI


Hivi ndivyo  mkazi  wa Wenda  alivyochunwa  ngozi na  watu  wasiojulikana (Tunaomba Radhi kwa  picha hizi )

Hii  ndio  nyumba  ulimokutwa mwili  wa  mkazi huyo

eneo la  tukio



Baada ya siku mbili mtandao huu kuripoti tukio la kusikitisha kilichohusisha mauaji ya kinyama ya dereva wa bodaboda sadiki mbelwa (26) katika kijiji cha wenda, Tanangozi Iringa ambapo mwili wa marehemu ulikutwa ukiwa na majeraha sehemu za kichwani huku ikisadikiwa kupigwa na kitu chenye ncha kali.
eo katika tukio lingine la kusikitisha ambalo limetokea katika kijiji cha wenda kitongoji cha Lupeta amekutwa mwili mwanakijiji aliyetambulika kwa jina la Leornad Kutika (49.

Mwili wa marehemu kutika umekutwa katika nyumba aliyokuwa akiishi huku ukiwa umechunwa ngozi, kunyofolewa macho pamoja na kukatwa sehemu za siri.

Akingea na mtandao huu wa huzuni baba mdogo wa marehemu Martin Kutika mkazi wa lupeta anaeleza kuwa usiku wa kuamkia jana alipigiwa simu ndugu wa marehemu aliyefahamika kwa jina Kibadeni kutika kuwa ndugu yake huyo ambayekwa mujibu wa maeezo yake alikuwa akisumbuliwa na tatizo la akili alikutwa katika nyumba aliyokuwa anaishi huku akiwa amefariki na kuondolewa sehemu za siri na kuchunwa ngozi. Zwadi mwenga ambaye pia ni ndugu wa marehemu anaeleza kuwa alipata taarifa za tukio hilo jana na ndipo alipofika katika nyumba ya marehemu na kukuta akiwa amefariki.

Akilelezea kuhusu tatizo alilokuwa nalo marehemu Mwenga amesema marehemu alianza kusumbuliwa na tatizo la kurukwa akili tangu alipokuwa mdogo japo hakuwahi kufanya vurugu yoyote na wao kama familia wamekuwa wakimpatia chakula na siku mbili kabla ya tukio marehemu alionekana lakini baada ya hapo hawakumuona tenda ndipo wifi yake alipofika nakukuta marehemu amekufa huku akiwa ametendewa unyama huo.
 Afisa mtendaji wa kijiji cha wenda Dismas Ngweta anaeleza kuwa alipigiwa simu na mwenyekiti wa kjjij cha lupeta Geofrey Dugange nakumweleza kuwa hakuna amani katika kijiji hicho kuwa kuna mwanankijiji ambaye ameuawa. Akielezea baada ya kufika eneo la tukio Ngweta anaeleza kuwa walipouangalia mwili wa marehemu waligundua kuwa amechunwa ngozi, kunyofolewa macho, kukatwa sehemu za siri pamoja na kutobolewa katika sehemu ya mguu. Akilinganisha tukio hili na lililotokea siku chache zilizopita Ngweta ameeleza kuwa tukio la dereva wa bodaboda limetokea wakati wa usiku na kusema kuwa inasemekana kuwa tukio la pili limetendeka usiku kwani kwa mujibu wa wanakiji walieleza kumwona marehemu jioni kabla ya tukio.

 Je nijuhudi gani zimefanywa na jeshi la polisi mpaka sasa? Ngweta ameeleza kuwa baada ya kupata taarifa ya tukio hilo alipiga simu kwa mkuu wa kituo cha ifunda naye akajibu kuwa awasiliana na wa kituo kikubwa Iringa. Mpaka mtandao huu unatoka eneo la tukio hakuna afisa usalama aliyekuwa amefika katika eneo hilo.

Tukio hili ni la mara ya pili kutokea baada ya tarehe 25 Septemba kuripotiwa kuuwawa kinyama kwa dereva wa bodaboda na pikipiki yake kutoonekana.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog