Home » »

MADAM RUTI ALIA NA MAKANISA



Mwimbaji wa muziki wa injili nchini, Madamu Ruti Mwamfupe amedai kulizwa na makanisa yanayoshindwa kuwasaidia watu wenye uhitaji kama wagonjwa waliolazwa hospitalini.

Akizungumza  Dar es salaam jana, Madamu Ruti alisema hospitalini kuna baadhi ya watu ambao hawana fedha za kununua hata chakula, wakati watumishi wa Mungu wanakula na kusaza.''
Hata vitabu vitakatifu vinasema; dini iliyosafi isiyo taka mbele za Mungu Baba ni hii, kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao ya kujilinda na dunia,'' alisema Madamu.

Mwimbaji huyo alisema, endapo makanisa hayo yangejiwekea utaratibu wa kuwasaidia wagonjwa kila wiki, ingewawezesha baadhi yao kupona haraka. Alisema wagonjwa wengi wanachelewa kupata uponyaji kutokana na kushindwa kupata mlo bora, licha ya kutumia dawa zinazohitaji kula chakula kingi.

Mwimbaji huyo hivi karibuni alikwenda kutembelea wagonjwa katika hospitali ya Ocean Road na kutoa misaada ya vitu mbalimbali, vyenye thamani ya sh. 700,000 na fedha taslimu sh. 500,000.

Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog