Home » »

MASHABIKI WA PASTOR BENJAMIN DUBE WAACHWA NA SIMANZI NCHINI SWAZILAND

Pastor Benjamin Dube akimsifu Mungu katika moja ya recording zake.
                             
Mashabiki wa mwimbaji nguli wa muziki wa gospel pastor Benjamin Dube nchini Swaziland wamefikwa na huzuni baada ya onyesho lililokuwa limepangwa kufanyika katika uwanja wa trade fair hii leo kuahirishwa kutokana na wahusika waliotaka kumkaribisha mwimbaji huyo kushindwa kutimiza mahitaji hali iliyomfanya mwimbaji huyo kuwaomba radhi mashabiki wake na kuwataka kumsubiri hadi tarehe 10 mwezi November mwaka huu atakapokuwa na ziara nchini humo.

Licha ya ziara ya mwimbaji huyo ktokuwepo wikiendi hii huko Swaziland lakini taarifa alizozipata kutoka kwa mashabiki ni kwamba matangazo ya runinga kuhusiana na onyesho lake bado yanatangazwa jambo ambalo limemsononesha.

Mwimbaji huyo katika ratiba yake mwisho wa wiki hii  atakuwa katika mji wa Klerksdorp, Botswana na hapo kesho alitarajiwa kuhitimisha ziara yake huko Swaziland lakini sasa haitawezakana ambapo tayari amewaomba radhi mashabiki wake waliokuwa wakimsubiri kwa hamu.Lakini pia hakuacha kuwaambia wapenzi wake kuwa atakuwa nchini Lesotho mwezi ujao tarehe 28, pamoja na  kumshukuru Mungu kutokana na kazi nzuri waliyoifanya na kundi zima la Spirit of Praise ambao walirekodi album yao ya 4 septemba mosi wiki iliyopita.

Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog