Home » »

MCHUNGAJI PETER MSIGWA AENGULIWA KUWANIA UENYEKITI WA CHADEMA JIMBO LA IRINGA MJINI

Add caption
KUELEKEA UCHAGUZI WA CHADEMA IRINGA MJINI: Habari zisizo rasmi kutoka eneo la chumba cha mkutano mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) zimedai kwamba Mchungaji Peter Msigwa ameenguliwa kutetea nafasi yake ya uenyekiti.

Ameenguliwa kwa kile kilichoelezwa na wapashaji wetu kwamba anachangia kwa kiasi kikubwa kuongeza makundi ndani ya chama hicho.

Makundi hayo yanaelezwa kukiwekwa rehani chama hicho wakati kikijiandaa kwa Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Pamoja na Mchungaji Msigwa, taarifa hizo zimesema Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa, Chiku Abwao (Chadema) naye ameenguliwa kuwani nafasi yoyote ya uongozi katika chama hicho mkoani hapa.

Hivikaribuni Abwao alinukuliwa akitangaza kuwania nafasi ya uenyekiti wa mkoa wa chama hicho unaotarajia kufanyika Jumapili keshokutwa.

Kuenguliwa kwa Msigwa katika uchaguzi huo kumeacha kampuni wagombea wawili wanaomenyana katika nafsi hiyo itakayosaidia kutoa picha ya jinsi mambo yatakavyokuwa wakati wa mchakato wa kumpta mgombea ubunge jimbo la Iringa Mjini mwaka 2015.

Wagombea hao ni Frank Nyalusi anayeelezwa kuwa ni mfuasi wa kufa na kupona wa Mchungaji Peter Msigwa na Mohamed Makuke ambaye ni mfuasi wa kundi la wengi linalodaiwa kumpinga Mchunngaji Msigwa.

Kundi linalojiita la wengi katika chama hicho limesikika likisema mara kwa mra kwamba tabia ya Mchungaji Msigwa ndani ya chama hicho inawaweka katika wakati mgumu wa kutetea nafasi ya ubunge mwaka 2015.

Mchungaji Msigwa ni kiongozi asiyeambilika, anayejua kila kitu, mbishi, kaidi, mwenye kiburi, asiyependa watu, mwenye visasi, majivuno na asiyetaka ushirikiano toka kwa wenzake, asiye na mikakati ya kujenga chama huku akiamini siasa za kitaifa pekee anazopenda zaidi zinaweza kulinusuru jimbo hili katika Uchaguzi Mkuu wa mwakani.

Wakati Mchungaji Msigwa akirushiwa lawama zote hizo, taarifa za uhakika zimedai kwamba ofisi ya wilaya ya chama hicho imefungwa na wameamuliwa kuondoka baada ya uongozi wa mbunge huyo unaomaliza muda wake kushindwa kulipa kodi ya pango. Mchungaji Msigwa ndiye Mwenyekiti wa Chadema jimbo la Iringa Mjini anayemaliza muda wake hii leo.

Wanachama wa chama hicho wamechukizwa kwa hatua ya mbunge wao kuridhia kupoteza ofisi pekee ya chama hicho mjini Iringa kwasababu ya kushindwa kulipa Sh 540,000 walizokuwa wakidaiwa.

Matokeo ya uchaguzi huo yanatarajiwa kutangaza baadaye hii leo.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Search This Blog