AJALI YA GARI YAUA WATU 6 NA KUJERUHU VIBAYA WENGINE 18 HUKO MKOANI RUVUMA
WATU
sita ambao ni abiria waliokuwa wakisafiri kwa basi kutoka Mbinga mjini
kwenda makao makuu ya wilaya mpya ya Nyasa, mkoani Ruvuma wamefariki
dunia na wengine 18 kujeruhiwa vibaya baada ya gari hilo walilokuwa
wamepanda, kuacha njia na kutumbukia kwenye korongo.
Akizungumza
na Mwandishi wa habari hizi, Kamanda wa Polisi wa mkoa huo Mihayo
Msikhela, alisema gari hilo lenye namba za usajili T 759 BVR aina ya
Nissan Civillian lilipata ajali Agosti Mosi mwaka huu, majira ya saa
10:30 jioni katika kijiji cha Burma kata ya Nyoni wilayani Mbinga.
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Ruvuma Mihayo Msikhela akimtaka hali mmoja kati ya majeruhi Joseph Matembo aliyelazwa katika hospitali ya wilaya ya Mbinga |
Mihayo
alifafanua kuwa ajali hiyo ilisababishwa na gari kuwa katika mwendo
kasi, ambapo dereva aliyekuwa akiliendesha alishindwa kulimudu kwenye
kona kali na hatimaye lilitumbukia katika shimo kubwa (korongo) na
kusababisha mauaji na majeruhi hao.
“Mpaka
sasa dereva aliyekuwa akiliendesha gari hili bado jina lake halifahamiki
kutokana na kukimbia kusikojulikana, Jeshi la polisi tunafanya jitihada
ya kumtafuta ili aweze kupatikana na baadaye tupate maelezo yakinifu
juu ya tukio hili”, alisema Mihayo.
Aliwataja
walimu wa shule ya msingi waliofariki dunia kuwa ni Esther Kumburu wa
shule Kilimani wilayani Mbinga na Efigenia Kayombe ambaye ni mwalimu wa
shule ya Linda iliyopo Mbambabay wilayani Nyasa.
Vilevile
kulikuwa na Ernest Ndunguru mkazi wa kijiji cha Mikalanga wilayani
Mbinga, Anna Chitete kijiji cha Kilosa wilayani Nyasa na mmoja ambaye
alifahamika kwa jina moja la Mbunda mkazi wa kitongoji cha Lusonga
Mbinga mjini, na kwamba maiti moja ambaye ni wa kiume bado hajatambuliwa
jina lake mpaka sasa.
Aidha
Kamanda Mihayo alieleza kuwa maiti zote zimehifadhiwa katika hospitali
ya wilaya ya Mbinga, na kwamba majeruhi bado wanaendelea kupatiwa
matibabu katika hospitali hiyo lakini hali zao bado ni mbaya.
Hata
hivyo alitoa wito kwa madereva wote mkoani Ruvuma, kuacha kuendesha
vyombo vya moto barabarani kwa mwendo kasi, ikiwemo vile ambavyo
vimekuwa vikibeba abiria kwani kufanya hivyo kuna hatarisha maisha ya
watu wanaosafiri, kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Kwa uupande wake mkuuu wa wilaya ya mbinga Senyi Ngaga alipohojiwa na jamvilahabari kwa njia ya simu kuhusina na ajali iliyotokea alieleza kuwa taarifa hiyo ameipata akiwa Jijini Dar es salaam kwa shughuli za kikazi lakini hawezi kuongea chochote kwa sababu yupo nje ya wailaya hiyo.
“Mwandishi
labda umtafute kaimu mkuu wa wilaya ambaye nimemwachia wilaya hiyo
kwani yeye ndiye atakuwa na maelezo mengi ya wilaya hiyo ila sasa hivyo
yupo mbeya kwenye mkutanao wa wawekezaji alisema Senyi”
Hata hivyo kaimu mkuu wa wilaya hiyo ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya songea Joseph Joseph Mkirikiti alipohojiwa na jamvilahabari kwa njia ya simu alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo alidai kuwa imetokea katika kijiji cha Burma kwenye eneo la mlima chunya ambapo gari hilo lilikuwa linatoka Mbinga kwenda Mbambabay.
0 comments:
Post a Comment