Home » »

MCHUNGAJI MWASUMBI AACHILIWA HURU BAADA YA HUKUMU YA MIAKA 30 JELA KWA TUHUMA ZA UBAKAJI, MAGEREZA WALIA KUMKOSA MHUBIRI WAO

Mchungaji Mwasumbi akiwa mahakamani mwaka jana.
Hatimaye Mchungaji Daniel Mwasumbi ambaye mwaka jana alihukumiwa na Mahakama ya Wilaya ya Mbeya kifungo cha miaka thelathini (30) jela Julai mwaka 2013 kwa tuhuma za ubakaji hapo jana tarehe 3 Juni ameachiwa huru na Mahakama kuu kanda ya Mbeya  huku akiwa anatetewa na wakili wa kujitegemea Benjamini Mwakagamba mbele ya jaji Atuganile Ngwala, huku upande wa serikali ukiwakilishwa na Prosista Paul.

Kwa mujibu wa WAPO Radio FM 98.1 kupitia kipindi cha Yaliyotokea kinachorushwa saa moja usiku, ripota kutoka mkoani Mbeya bwana Ezekiel Kamanga ambaye alifika mahakamani hapo, anasema kwa upande wa utetezi wakili Benjamini Mwakagamba aliwasilisha sababu saba ambazo zilikuwa zikiomba mahakama hiyo kumwachia huru kutokana na hakimu kukosea kuzingatia moja ya mashahidi ambaye alikuwa ni shahidi wa kwanza.

Ameongeza kuwa pili ni kuwa hakimu alikuwa ameegemea ushahidi wa upande mmoja tu hivyo mahakama haikuwa na haki ya kumfunga kifungo hicho cha miaka thelathini . La tatu ni kuwa hakimu alitumia maoni yake binafsi kumfunga mshtakiwa hali ambayo ni kinyume cha sheria. Sababu ya nne ambayo ilitolewa na upande wa utetezi ni kutumika kwa kivuli cha kadi ya kliniki hali ambayo haikuwa ni halali kuweza kuwakilisha kama upande wa ushahidi.

Lakini  sababu nyingine ni kuhusu kuchelewa kwa vipimo vya DNA kutumwa jijini Dar es Salaam huku pia sababu nyingine ikielezwakuwa kubwa ni kukosewa au kutozingatia muda wa kesi hiyo mara baada ya kufikishwa polisi kutumia mda mrefu tangu kukamatwa, kwani ilichukua takribani miezi minne ndipo alipokamatwa mtuhumiwa hali ambayo mahakama ilitilia shaka na hivyo kwa upande wake jaji Atuganile Ngwala kuamua kumwachia huru kutokana na sababu hiyo ni kwamba hivi sasa mchungaji Daniel Mwasumbi atakuwa huru  ambapo kesi hiyo ya rufaa namba 59  ya mwaka 2013 ikimalizikia hapo, ali iliyopelekea watoto wa Mchungaji Daniel Mwasumbi kuangua kilio cha furaha mahakamani.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog