Home » »

HAKIKA MUNGU NI MWAMINIFU NA AHADI ZAKE NI ZA MILELE MWANAMKE SUDAN ALIYEHUKUMIWA KIFO, KUACHILIWA HURU


Afisa mmoja mwandamizi katika wizara ya maswala ya kigeni nchini Sudan amesema kuwa mwanamke aliyepewa hukumu ya kifo kwa kubadili dini yake ya kiislamu,Meriam Ibrahim atawachiliwa huru katika kipindi cha siku chache zijazo.

Abdullahi Alzareg ambaye ni katibu katika wizara hiyo amesema kuwa Sudan inatilia maanani uhuru wa kuabudu na kwamba serikali itamtetea mwananmke huyo.

Kumekuwa na shutma za kimataifa kuhusu hukumu aliyopewa mwanamke huyo.

Meriam Ibrahim anazuiliwa katika jela moja ambapo alijifungua mtoto wa kike juma hili.

Ameolewa na mkristo na pia amehukumiwa kuchapwa viboko mia moja kwa kuzini kwa sababu mwanamke wa kiislamu kuolewa na mkristo ni haramu kulingana na sheria za Sudan.

chanzo BBC Swahili.

Soma HAPA ZAIDI 

Daniel akiwa amembeba motto wake aliyezaliwa wiki iliyopita.
Meriam akiwa amebeba motto wake aliyejifungua huko gerezani
Meriam na mumewe, pembeni mtoto wao wa kiume anayeishi naye jela.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog