Home » »

Watu kadhaa wamehofiwa kufariki kufuatia mlipuko uliotokea ndani ya gari moja dogo la abiria katika mtaa wa Pangani mjini Nairobi.
Duru zinaarifu kuwa karibu watu 4 huenda wamefriki katika shambulizi hilo na wengine kadhaa kujeruhiwa.
Shirika la msalaba mwekundu limesema kuwa watu 15 waliojeruhiwa walipelekwa hospitalini.
Hata hivyo polisi hawajatangaza idadi rasmi ya watu waliojeruhiwa wala wale waliofariki.
Mlipuko huo umesemekana kutokea ndani ya matatu iliyokuwa inakwenda katika mtaa wa Eastleigh ambao una idadi kubwa ya wasomali wanaoishi huko.
Athari za mlipuko huo hazikuyasaza magari mengine manne yaliyokuwa karibu na matatu hiyo.
Polisi walilazimika kutumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya watu waliokusanyika katika eneo la shambulizi kujionea yaliyokuwa yanajiri.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog