Home » »

BALE APIGA HAT-TRICK REAL IKIUA 4-0 NA KUISOGELEA BARCA MGONGONI KABISA LA LIGA

WINGA Gareth Bale jana amefunga mabao matatu peke yake yaani hat-trick wakati Real Madrid ikiitandika Valladolid 4-0 Uwanja wa Bernabeu, Madrid na kuisogelea Barcelona kileleni mwa La Liga ikibaki inazidiwa pointi tatu.
Mchezaji huyo ghali wa dunia ameendelea kutekeleza vyema majukumu ya Cristiano Ronaldo ambaye ni majeruhi kwa sasa akiwa ametimiza mabao tisa katika mechi 13.Bale aliyefunga mabao hayo katika dakika za 33, 64 na 89 huku lingine liifungwa na Karim Benzema dakika ua 36, anakuwa mchezaji wa pili wa Uingereza kufunga hat-trick katika La Liga akimfuatia Gary Lineker mwaka 1987.
Real Madrid: Lopez, Carvajal, Pepe, Ramos, Marcelo, Alonso, Modric, Di Maria, Isco, Bale na Benzema.
Real Valladolid: Marino, Alcatraz, Rueda, Valiente, Pena, Rubio, Sastre, Rossi, Larsson, Guerray na Bergdich.
La kwanza: Winga wa Real Madrid, Gareth Bale akishangilia bao lake la kwanza Uwanja wa Bernabeu jana
Stuck in: Bale vies for possession with Valladolid's forward Javi Guerra
Bale akimtoka mshambuliaji wa Valladolid, Javi Guerra
Tight at the top: Bale helped Real Madrid narrow the gap at the top of La Liga to three points
Bale ameisaidia Real Madrid kupunguza la pointi La Liga wanazozidiwa na vinara Barcelona hadi kubaki tatu
 
 
 
 
GGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGGG
 

ARSENAL HAIKAMATIKI BWANA WEEEE, YAWAFUMUA CARDIFF 3-0 BARAZANI KWAO...LUKAKU NI HATAREEE

London, England
ARSENAL imezidi kijichimbia kileleni mwa Ligi Kuu ya England, baada ya kuilaza mabao 3-0 Cardiff City, kwenye Uwanja wa Cardiff jioni hii.
Mabao ya Arsenal yamefungwa na Aaron Ramsey dakika ya 29 akimalizia pasi ya Mesut Ozil na 90 pasi ya Theo Walcott na Mathieu Flamini dakika ya 86 pasi ya Ozil tena. 
Ushindi huo, unaifanya Arsenal itemize pointi 31 baada ya kucheza mechi 13, ikiizidi Liverpool iliyo katika nafasi ya pili kwa pointi saba. 
Ramsey hakutaka kushangilia baada ya kuifunga timu yake ya zamani

Katika mechi nyingine za Ligi Kuu England leo, 
Everton imeichapa 4-0 Stoke City Uwanja wa Goodison Park mjini Liverpool, mabao ya Gerard Deulofeu dakika ya 45, pasi ya Gareth Barry, Seamus Coleman dakika ya 49 pasi ya Barry tena, Bryan Oviedo dakika ya 58, pasi ya Gerard Deulofeu na Romelu Lukaku dakika ya 79 pasi ya Oviedo.
Bao pekee la Gary Hooper dakika ya 30 limeipa Norwich ushindi wa 1-0 dhidi ya Crystal Palace Uwanja wa Carrow Road, Norwich, Norfolk.
Lukaku akishangilia bao lake leo

West HamUnited imeifunga 3-0 Fulham Uwanja wa Boleyn Ground, London mabao ya Mohamed Diame dakika ya 47, Carlton Michael Cole Okirie dakika ya 82 na Joe Cole dakika ya 88.
Aston Villa imetoka sare ya bila kufungana na Sunderland Uwanja wa Villa Park na mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu England, Newcastle United wataikaribisha West Bromwich saa 5:30 usiku. 



HHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHH

KENYA WAOTEA VIBONDE, WAWACHAPA 3-1 NYAYO

Na Mahmoud Zubeiry, Nairobi
KENYA imeshinda mechi ya kwanza Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge baada ya kuilaza Sudan Kusini mabao 3-1 kwenye Uwanja wa Nyayo, Nairobi jioni hii katika mchezo wa Kundi A.
Ushindi huo unaifanya Harambee Stars ifikishe pointi nne baada ya awali kutoa sare ya bila kufungana na Ethiopia katika mchezo wa ufunguzi.
Joackins Atudo aliifungia Kenya bao la kwanza dakika ya 16 kwa penalti, baada ya beki mmoja wa Sudan Kusini kuunawa mpira kwenye eneo la hatari.
Wachezaji wa Kenya wakimpongeza mfungaji wa bao lao tatu, David Owino leo Nyayo

Sudan Kusini ilisawazisha dakika ya 26 kupitia kwa Nahodha wao, Richard Jistin aliyepiga shuti kali la mpira wa adhabu umbali wa mita 25 ambalo lilimshinda kipa Duncan Ochieng.
Jacob Keli aliifungia Harambee bao la pili dakika ya 29 akiunganisha krosi ya Allan Wanga kutoka upande wa kulia.
Atudo alikosa penalti dakika ya 70, baada ya kipa wa Sudan Kusini, Juma Jinaro kumuangusha Jacob Keli akiwa anakwenda kufunga. 
David Owino aliifungia Harambee bao la tatu dakika ya 78 baada ya kuwatoka mabeki wa Sudan Kusini.   
Matokeo haya yanamaanisha Kenya na Ethiopia sasa zinalingana kwa kila kitu, pointi nne kila mmoja, mabao matatu ya kufunga na bao moja la kufungwa, wakati Zanzibar sasa ni ya tatu kwa pointi zake tatu na Sudan Kusini inashika mkia.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog