Home » »

WANANCHI RUKWA WATEKETEZA SHAMBA LINALOMILIKIWA NA KANISA LA EFATHA

Shamba la Malonje linalomilikiwa na Kanisa la Efatha limepata hasara kubwa baada ya wananchi wa kijiji cha Sikaungu wilayani Sumbawanga vijijini mkoani Rukwa, kujichukulia sheria mkononi na kuvamia moja ya kambi ya mashamba hayo ijulikanayo kama sikaungu na kuyateketeza kabisa matrekta mawili makubwa mawili aina ya New Holland na kubomoa baadhi ya nyumba zilizopo katika kambi hiyo.

Mchungaji kiongozi Michael Meela wa kanisa la Efatha mkoani Rukwa akiongelea kuhusu suala hilo amesema hasara iliyopatikana kutokana na tukio hilo ni zaidi ya shilingi milioni 228 na tukio hilo lilitokea baada ya mbunge wa jimbo la Kwela Mh. Ignas Malocha kuhutubia mkutano wa hadhara kijijini hapo na kuwahamasisha wanachi watumiee nguvu ya umma kuyakomboa mashamba yao yaliyochukuliwa na mwekezaji huyo.

Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog