Home » »

KANISA LA BETHEL PENTECOSTE BUZA NALO LAPATA KISANGA CHA MOTO

Wakati jeshi la polisi na lile la wananchi (JWTZ) waliweza kutuliza hali ya uvunjifu wa amani ikiwa pamoja na maandamano yaliyokuwa yamepengwa kufanywa na waumini wa dini ya kiislamu kuelekea ikulu ili kushinikiza kuachiwa huru kwa sheikh Ponda Issa Ponda na waumini wengine wa dini hiyo waliokamatwa kwa tuhuma za kuchochea vurugu za kidini nchini.

Huko Buza njia panda ya kuelekea Kitunda jijini Dar es salaam, watu wasiofahamika wamelichoma moto upande mmoja kanisa la Bethel Pentecoste linaloongozwa na mchungaji Emanuel Kapama majira ya usiku wakati waumini wakiwa tayari majumbani mwao.

Kwa mujibu wa mchungaji Kapama amesema jana walikuwa na ibada kuanzia majira ya saa 1 usiku hadi saa 2 kisha kutawanyika lakini waliporejea asubuhi wakashangaa kukuta kanisa lao limechomwa moto upande mmoja na kukuta chupa ya mafuta ya taa ambayo imechukuliwa na jeshi la polisi kwa  ushahidi ikiwa ndani ya kanisa hilo huku watu hao wakiwa wameshamwaga mafuta ya taa kanisa zima ambalo limezungushiwa kwa mabati pamoja na mifuko migumu aina ya viroba.

Ambapo kwa mujibu wa mchungaji huyo amesema jeshi la polisi tayari limefika na kuangalia kilichotokea na kuchukua vitu ambavyo vitatumika kwa ushahidi ikiwemo chupa hiyo ya mafuta ya taa.
Moja ya kanisa lililochomwa moto huko mkoani Kigoma wiki hii. picha by Fungo Omary.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog