Home » »

JE? MWIMBAJI WA ''MY GOD IS GOOD'' PASTOR UCHE AMEJITOA JOYOUS CELEBRATION?

Pastor Uche akiimba Solid Rock ndani ya Joyous 15 part 2.
Baada ya kuwemo ndani ya kundi la Joyous Celebration kwa takribani miaka 5, mwimbaji aliyejipatia umaarufu sana duniani ikiwa pamoja na kulitangaza vyema kundi hilo Pastor Agu Uchechukwu au unaweza kumuita Pastor Uche a.k.a Double double yawezekana album ya 16 ndio ilikuwa ya mwisho kwa mwimbaji huyo akiwa na kundi hilo.

Hali hii yakujiuliza maswali kama haya ni hivi karibuni JC imetangaza tarehe ya kurekodi album yao mpya ya 17 ambayo itafanyika mwezi December, mwimbaji Pastor Uche siku chache kabla kupitia katika moja ya kurasa zake za Facebook aliaga kwamba anaelekea nchini Marekani na kuongeza kuwa kurudi kwake nchini Afrika ya kusini hadi mwezi wa tatu mwakani 2013 jambo ambalo linatafsiri kama mwimbaji huyo hayumo tena kundini humo.

Tangu JC ianze tour ya kutangaza album yao ya 16, pastor Uche hakuweza kuhudhuria takribani maonyesho yote kutokana na mialiko anayoipata huko nchini Marekani. Ambapo kwasasa anapanga kurekodi DVD yake ya pili Live huko Houston nchini Marekani, kama ni kweli atakuwa ameachana na kundi hilo inamaanisha atakuwa amebakia kijana mzimbabwe Mkhululi anayeimba nyimbo zinazo kwenda sambamba na Uche au kundi hilo litakuwa mbioni kutafuta mtu wa kuchukua nafasi yake.

Moja ya ratiba zake alizoweka katika ukurasa wake wa FB inaonyesha kabisa kwamba hatarekodi album mpya na JC mwaka huu kwani siku ambayo kundi hilo linarekodi yeye atakuwa na show sehemu nyingine
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog