Home » » ASKOFU MKUU WA TANZANIA ASSEMBLIS AZINDUA MAABARA YA KISASA KATIKA SHULE YA SEMINARY EBENEZER MKOANI IRINGA

ASKOFU MKUU WA TANZANIA ASSEMBLIS AZINDUA MAABARA YA KISASA KATIKA SHULE YA SEMINARY EBENEZER MKOANI IRINGA

Wito umetolelewa kwa wanafunzi wanao hitimu kidato cha nne hapa nchini kuweza kuendeleza nidhamu zao hata baada ya kuhitimu kwani hiyo ndo njia pekee itakayowawezesha wanafunzi kufaulu na kukamilisha malengo yao ya hapo baadae.

Wito huo umetolewa na Askofu mkuu wa kanisa la Tanzania assemblia of god   Dr Barnabas Mtokambali katika mahafali ya tatu ya kidato cha nne ya shule ya seminary ebenezer iliyopo nduli jirani na uwanja wa ndege manispaa ya iringa.

Ambapo mbali na maafari hayo Askofu Mtokambali aliweza kuzindua rasmi maabara ya kisasa itakayo wasaidia wanafunzi wote wanaosoma masomo ya sayansi Mtokambali alisema iwapo wanafunzi watafuata nidhamu waliyofundishwa na kuionyesha  katika jamii zao hakika hakutakuwa na mwanafunzi wa kufeli hata mmoja kwa anaamini kuwa nidhamu ndio chanzo kikuu cha mafanikio.

Hata hivo alimpongeza mwalimu mkuu wa shule hiyo bw.makweta na kuaahidi kusaidiana katikachanga moto mbalimbali zinazohusu shule hiyo kama tatizo la maji ambapo askofu mkuu aliahidi million mbili katika kufanikisha na kutatua jambo hilo, na zaidi ya millioni sita zilichangiashwa katika kutatua sual;a la maji .

Kwa upande wake  mkuu wa shule ya ebenezer alimpongeza askofu mkuu pamja na uongozi wa jimbo  la iringa uliongozwa na Askofu Jonas Mkane pamoja na makamu wake Edward Tom Matipa kwa uwepo wao katika kufanikisha zoezi zima la mahaafari pamoja na uzinduzi wa maabara ya kisasa kwa wanafunzi wa shule hiyo.




Askofu mkuu wa tanzania assemblis of god wakati akiwasili katika shule ya ebenezer




Askofu mkuu wakati akizindua rasmi maabara ya kisasa


Asikofu  wa jimbo la iringa jonas mkane akifungua kwa maombi sherehe


makamu askofu wa jimbo la iringa rev edward tom matipa




baadhi ya majengo ya shule ya ebenezer seminary

wahitimu wakicheza kwaito kwa pamoja



Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog