Home » »

Mtoto ashukiwa kuwaambukiza wengi Mali

Shirika la afya duniani WHO linasema kwa msichana wa umri wa miaka miwili ambaye alithibitishwa kuwa mgonjwa wa kwanza wa ebola nchini Mali alisafiri kilomita kadha kwa basi nchini humo huku akionyesha dalili za kuugua ugonjwa huo.
Zaidi ya watu 40 ambao walikaribiana naye wametengwa. Huenda msichana huyo alisafirishwa kwenda nchini Mali na nyanyake baada ya mazishi ya mamake nchini Guinea moja ya nchi ambazo zimeathirka pakubwa na ugonjwa wa ebola.
Utawala nchini Mali sasa umethibitisha kuwa msichana huyo ameaga dunia kwenye hospitali moja mjini Mayes alikokuwa akipewa matibabu.
Mwandishi wa BBC anayehusika na masuala ya afya anasema kuwa huenda ikawa changamoto kubwa kuwapata watu wengine ambao walikaribiana na msichana huyo.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog