Bagamoyo mkoani Pwani kupitia
chama cha mapinduzi CCM, ameibuka kidedea kwa asilimia 86.61 katika
uchaguzi huo na kuwamwaga wagombea wengine kutoka vyama vinne vya
upinzani.
Matokeo hayo yametangazwa usiku wa kuamkia leo April 7 majira ya saa
nane usiku katika shule ya sekondari Chalinze na Msimamizi wa uchaguzi
huo Bw.Samwel Salianga ambapo amesema CCM – Ridhiwani Kikwete
amepata kura 20,828 sawa na 86.61%, Chadema -Mathayo Torongei amepata
kura 2,544 sawa na asilimia 10.58,CUF- Fabian Skauki 476 sawa na
asilimia 1.98,NRA Hussein Ramadhani kura 60 asilimia 0.25 huku AFP
Ramadhani Mgaya amepata kura 186 sawa na asilimia 0.59.
Salianga
amesema kati ya watu waliojiandikisha katika daftari la kudumu la
wapiga kura ni watu elfu 92,waliojitokeza katika zoezi hilo ni watu
24,422 ambapo kura halali zilikuwa 24,047 na kura 375 zikiharibika.
Wagombea waliokuwepo wakati wa kutangaza matokeo katika uchaguzi huo na kusaini fomu ya kukubalina na matokea alikuwepo mgombea wa NRA na CCM pekee.
Aidha Wakizungumza baada ya kupokea matokeo hayo aliyekuwa mgombea wa
chama cha NRA pamoja na Ridhiwani Kikwete kupitia CCM,kila Mmoja
ameshukuru wananchi na kuahidi kushirikina na wananchalinze kuleta
maendeleo.
0 comments:
Post a Comment