Home » »

UTAJIRI WA DHULUMA NA KAFARA HAUNA BARAKA WALA AMANI

Askofu Paul Akyoo. picha kwa hisani ya elct.org
Askofu Paul Akyoo wa Dayosisi ya Meru kanisa la Kilutheri nchini amekemea vikali utajiri wa dhuluma na kafara kwakuwa hauna baraka. Askofu Akyoo ameyasema hayo hapo jana wakati wa ibada ya mazishi ya mfanyabiashara maarufu wa madini ya Tanzanite jijini Arusha marehemu Erasto Msuya aliyefariki kwakupigwa risasi Agosti 7 mwaka huu.

Askofu Akyoo katika mahubiri yake alisema utajiri wa dhuluma na kafara hauna baraka wala amani kwa wahusika kutokana na dhamira zao kuwasuta kila wanapokumbuka uhalifu walioutenda. Aidha kwa upande wa mkuu wa mkoa Arusha Magesa Mulongo akisema “Waliomuua Msuya wataumbuka mchana kweupe wiki ijayo watakapofikishwa mahakamani. Nawahakikishia kuwa vyombo vya dola viko kazini na ukweli kuhusu waliohusika na tukio hili la kinyama utajulikana hadharani wiki ijayo wahusika watakapofikishwa mahakamani,” alisema Mulongo katika ibada hiyo.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog