Home » »

MSIBA WA ASKOFU KULOLA KUWA EAGT TEMEKE, MWILI KUSAFIRISHWA MWANZA, FLORA MBASHA AZIMIA

Taarifa za mwendelezo kuhusu msiba wa Askofu Dr. Moses Kulola zinasema kuwa msiba utakuwa kanisa la EAGT Temeke kwa Mchungaji Ngowi, mahali ambapo kila mwaka amekuwa akifanya mkutano wa injili, na kwamba kwa wale ambao watapenda kuhudhuria wafike mahali hapo.
Mwili wa Askofu Kulola tayari umehamishwa kutoka hospitali ya AMI kwenda Hospitali ya Kumbukumbu ya Hurbet Kairuki iliyopo Mbezi jijini Dar. Mwili utasafirishwa kuelekea Mwanza, na mipango ya shughuli hiyo bado inafanyika.

Kwa mujibu wa Emmanuel Mbasha, mume wa Flora Mbasha (mjukuu wa marehemu Kulola) ameieleza Gospel Kitaa kuwa maandalizi bado yanaendelea na taarifa rasmi aitaendelea kutolewa kwa kadri ya muda unavyosonga.

Na taarifa ambazo zimefika hivi punde zinaeleza kuwa mjukuu wa Moses Kulola, Flora Mbasha, amezimia kwa muda sasa na anashughulikiwa na madaktari hospitalini, maombi yako yanahitajika ili apate kurejea kwenye hali ya kawaida.

Una habari kuwa Askofu Kulola hakuwahi kunyoa nywele tokea mwaka 1966? Bofya hapa ili kujua
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog