MSIBA WA ASKOFU KULOLA KUWA EAGT TEMEKE, MWILI KUSAFIRISHWA MWANZA, FLORA MBASHA AZIMIA
Mwili wa Askofu Kulola tayari umehamishwa kutoka hospitali ya AMI kwenda
Hospitali ya Kumbukumbu ya Hurbet Kairuki iliyopo Mbezi jijini Dar.
Mwili utasafirishwa kuelekea Mwanza, na mipango ya shughuli hiyo bado
inafanyika.
Kwa mujibu wa Emmanuel Mbasha, mume wa Flora Mbasha (mjukuu wa marehemu
Kulola) ameieleza Gospel Kitaa kuwa maandalizi bado yanaendelea na
taarifa rasmi aitaendelea kutolewa kwa kadri ya muda unavyosonga.
Na taarifa ambazo zimefika hivi punde zinaeleza kuwa mjukuu wa Moses Kulola, Flora Mbasha, amezimia kwa muda sasa na anashughulikiwa na madaktari hospitalini, maombi yako yanahitajika ili apate kurejea kwenye hali ya kawaida.
Na taarifa ambazo zimefika hivi punde zinaeleza kuwa mjukuu wa Moses Kulola, Flora Mbasha, amezimia kwa muda sasa na anashughulikiwa na madaktari hospitalini, maombi yako yanahitajika ili apate kurejea kwenye hali ya kawaida.
0 comments:
Post a Comment