Home » »

UPENDO KILAHIRO NA CHRISTINA SHUSHO WAPO NCHINI CANADA KIHUDUMA


Baada ya kazi njema ya kumtukuza Mungu katika mkutano mkubwa wa injili nchini Canada ulioandaliwa na askofu Zachary Kakobe, waimbaji nyota wa gospel nchini Christina Shusho pamoja na Upendo Kilahiro bado wanaendelea na huduma ya injili nchini humo kabla ya kuelekea nchini Marekani kuendeleza moto wa injili.

Katika mawasiliano na GI,Upendo amesema wanamshukuru Mungu mkutano ulikuwa wa baraka sana, ambapo kwasasa wanajiandaa kwaajili ya tamasha kubwa la uimbaji tarehe 7/7/2013 huko Ottawa katika jengo la Wells of Salvation Church kwa anuani ya Venue 1401 Blair Place, tarehe 14 July wanatarajiwa kuwa katika mji wa Quebec. kisha wataelekea nchini Marekani. Waimbaji hao wamewakaribisha watu wote kutoka Afrika Mashariki na sehemu nyinginezo kufika katika mahali watakapohudumu.


Upendo Kilahiro ameachia album mpya hivi karibuni ikijulikana kwa jina la "Sinzog'igo Ntinya" huku Christina Shusho akiwa anaachia album nyingine iitwayo "Nataka Nimjue", waimbaji hao kwa pamoja wamekuwa wakifanya vizuri katika tasnia ya muziki wa gospel nchini kwa muda mrefu ikiwa pamoja na kupata mialiko mingi ndani na nje ya nchi.



Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Search This Blog