IGIZO LA YESU LATIKISA JIJI LA LONDON KWA MARA NYINGINE
Maelfu ya wakazi wa jiji la London nchini Uingereza pamoja na wageni
wake hapo jana walifurika katika eneo la wazi maarufu katikati ya jiji
hilo la Trafalgar Square kushuhudia igizo la Yesu ambalo hufanyika
takribani kila Ijumaa kuu ya kila mwaka katika eneo hilo tangu mwaka
2010, ili kukumbuka mateso aliyopata mkombozi wa ulimwengu Yesu Kristo
miaka 2000 iliyopita.
Igizo hilo lililoandaliwa na kuongozwa na Peter Hutley OBE KSG huku
kinara mwigizaji katika nafasi ya Yesu akiwa ni bwana James(jina moja tu
ambalo GK iliambulia kulipata kutoka kwa mwigizaji mwenyewe). Ambapo
muonekano wake hana tofauti na mwigizaji mkongwe katika sinema ya Yesu
(Jesus) Brian Deacon, watu waliohudhuria eneo hilo walionekana kwenda
sambasamba na waigizaji kwakuonyesha hisia zapo kulingana na uigizaji wa
wahusika.
0 comments:
Post a Comment