Home » »

BREAKING NEWS:MUME AUA MTOTO NA KUMCHOMA CHOMA MKE KWA KISU IRINGA

Bi Janeth akiongea na mwandishi wa habari
 Mwanaume mmoja mkazi wa ilolo mpya pawaga aliyetambulika kwa jina la Isaya Samamba,amejikuta hatiani baada ya kumuua kwa kumchomachoma mtoto wake Vanesa wa miezi kumi kwa kisu na kumjeruhi mama wa mtoto huyo anayetambulika kwa jina la Janeth malenda,akiongea na mtandao huu Bi.Janeth amesema kuwa siku hiyo alikuwa ameenda katika mkutano wa Injili na aliporudi nyumbani giza lilikuwa tayari limeingia,walipokuwa chumbani yeye,mtoto pamoja na mumewe alishangaa kuona ghafla mumewe akimchoma kwa kisu ndipo alipoamua kukimbia nnje na kupiga kelele ili wasamalia wema waje wamsaidie baada ya watu kufika walikuta mtuhumiwa amekimbia huku wakishuhudia mwili wa mtoto ukiwa umejaa damu na utumbo ukiwa nnje.
 Watu waliofika walichukua hatua na kutoa taarifa polisi na ndipo polisi walianza jitihada za kumsaka mtuhumiwa na alikamatwa usiku wa manane katika nyumba aliyofanyia mauaji akitaka kuchukua baadhi ya vitu ili atoroke  na kufikishwa katika kituo kikuu cha polisi Iringa. 
Mtandao huu unampa pole Bi.Janeth ambaye kwa sasa amelazwa hospitali ya mkoa iringa kwa matibabu zaidi.


Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Search This Blog