Home » »

MAMIA WAMIMINIKA KATIKA KONGAMANO LA MAOMBI NA MAOMBEZI KWA KATUNZI

Mamia ya wakazi wa jiji la Dar es salaam na vitongoji vyake wanamiminika katika kongamano kubwa la maombi na maombezi lililoandaliwa na kanisa la E.A.G.T City Centre chini ya mchungaji wake kiongozi Florian Katunzi katika ukumbi wa PTA uliopo viwanja vya mwalimu JK Nyerere zamani Sabasaba.

Kongamano hilo la siku nane lililoanza siku ya jumapili nakutarajiwa kumalizika jumapili hii linatarajia kupambwa na waimbaji mbalimbali wa gospel nchini wakiongozwa na Bahati Bukuku, Masanja Mkandamizaji, Flora Mbasha, Martha Mwaipaja, Solomon Mukubwa, Madam Ruti, Bonny Mwaitege na waimbaji wengine lukuki zikiwemo kwaya za kanisa hilo.

Ambapo toka jumapili tayari uwepo wa Mungu umeanza kujidhihirisha ukumbini hapo kwa watu mbalimbali kupokea uponyaji na kufunguliwa kutoka katika vifungo mbalimbali vya ibilisi ambapo kwa watu wasiofika katika ukumbi huo wanapata yanayojiri kwakusikiliza Wapo Radio FM inayorusha matangazo ya moja kwa moja kutoka ukumbini hapo.

  CHEKI BAADHI YA PICHA KUTOKA KATIKA KONGAMANO HILO TOKA LILIPOANZA.
Mchungaji Florian Katunzi akiwaongoza mamia ya wakazi wa jiji la Dar katika maombi.
Solomon Mukubwa kutoka Kenya akiita uwepo wa Mungu katika kongamano hilo.

Martha Mwaipaja wa John Saidi akimtukuza Mungu.
Solomon Mukubwa akimpiga picha Martha Mwaipaja wakati akiimba.
Picha ya Juu ni Waimbaji Madam Ruth pamoja na Martha Mwaipaja wakiwa na Solomoni Mukubwa kwa Pamoja wakimsikiliza Mtumishi wa Mungu wa Mungu Mchungaji Frolian Katunzi wakati akitamka Neno la Baraka kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam.
Mchungaji mtarajiwa a.k.a Masanja Mkandamizaji akipiga gombo la uimbaji katika kongamano hilo.
Sio utangazaji tu hata uimbaji ni balaa, anaitwa Silas Mbise ambaye pia ni mtangazaji wa Wapo Radio Fm akimtukuza Mungu katika kongamano hilo,
Flora Mbasha na mumewe mpenzi Emanuel Mbasha wakimsifu Mungu kwa pamoja.
Eveline Msoome nayeye hakuwa mbali katika kumsifu Mungu.
Kijana mwenye mavocal Samuel Limbu akimsifu Mungu katika kongamano hilo.
Mchungaji Yohana Mwegoha akimsifu Mungu. picha kwa hisani ya Yonathanlanda.blogspot.com
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Search This Blog