Home » » MZEE MWENYE WATOTO 100 ATAKA KUZAA ZAIDI ILI AZIKWE VIZURI AKIFA

MZEE MWENYE WATOTO 100 ATAKA KUZAA ZAIDI ILI AZIKWE VIZURI AKIFA

Kofi Asilenu mwenye umri wa miaka 80 ni baba wa watoto 100 na wake 12.


Wakati ulimwengu ulipoadhimisha siku ya idadi ya watu duniani mwanaume mmoja alikuwa na sababu 100 za kusherehekea.
Kofi Asilenu mwenye umri wa miaka 80 ni baba wa watoto 100 na wake 12.
Anaishi na familia yake katika kijiji cha Amankrom kilicho umbali wa kilomita 45 kutoka mji mkuu Acca.
Familia yake ni thuluthi moja ya watu 600 katika kijiji hicho.
Anasema kuwa anataka familia kubwa kwa sababu hana ndugu.
Sina kaka wala shangazi,ndiyo sababu niliamua kuwa na watoto wengi ndiyo wapate kunipa maziko yaliyo mazuri nikifa.
Familia hiyo yake hata hivyo imemgharimu pakubwa. anasema alikuwa mtu mwenye mali, lakini mali hiyo ilipungua kutokana na gharama ya kuitunza familia yake kubwa
Kofi Asilenu anaonekama kuwa mwenye afya nzuri na hata anasema anataka kuwa na watoto zaidi.
Via>>BBC
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Search This Blog