Home » »

DAS JOSEPH CHINTIKA: ISMANI HAKUNA NJAA

 Katibu tawala wa wilaya ya Iringa Joseph Chintika akizungumza na waandishi wa habari ofisni kwake.

 
Na Fredy Mgunda,Iringa

KATIBU tawala wa wilaya ya Iringa Joseph Chintika amesema kuwa tarafa ya ismani haina njaa kama ambavyo maneno yanayozagaa mitaani kuwa ukanda wa ismani kuwa kuna njaa.
Akizungumza na blog hii Chintika alisema kuwa kumekuwa na wanasiasa wanaoeneza kuwa tarafa ya ismani kuna njaa wakati hali halisi sio hiyo na kuongeza kuwa eneo hilo linachakula cha kutosha na hakuna tatizo la njaa.
“Angalia mvua zinanyesha kwa wingi na wananchi wamelima kwa wingi na mazao yanakuwa vizuri hivyo ismani hakuna njaa na sijapokea taarifa yoyote ile ya kuwepo kwa njaa kwa kuwa nimekuwa nikifanya ziara katika maeneo hayo mara kwa mara na nimejihakikishia kuwa hakuina njaa hali ya chakula ni nzuri na kuwaomba wananchi kuacha kuwasikiliza wanasiasa”.alisema Chintika
Chintika aliwataka wananchi kuacha kutumia mazao ya mahindi,mtama na uwele kupikia pombe kwa kuwa kufanya hivyo kutapunguza uwepo wa chakula katika eneo hilo.
Unakuta mtu anashawishiwa kuuza mahindi kwa mpika pombe wakatyi anajua kuwa hana chakula cha kutosha nasema ni marufuku kwa wananchi kupika pombe kwa kutumia mahindi,uwele na mtama ili  kuendelea kutunza chakula hicho.
Aidha Chintika alisema kuwa sasa ni fursa kwa wafanyabiasha kuuza mahindi katika maeneo mbalimba ya wilaya ya iringa kwa kuwa bei ya mahindi kwa sasa ni nzuri.
Hivi hawa wanansiasa wanayatoa wapi maneno ya uongo kuwa ismani kuna njaa naomba waje na takwimu na sio kuposha wananchi serikali ndio inaweza kutangaza kama sehemu kuna njaa na sio mtu mwingine yoyote.
“Serikali ndio chombo cha mwisho kuthibitisha kuwa ismani kuna njaa sio kila mtu anaweza kuongelea mambo ya serikali naomba hawa wanansiasa waache mara moja kupotosha wananchi na wakiendelea kupotosha jamii tutawachukulia hatua za kisheria maana hatuna tatizo la chakula katika tarafa ya ismani”.alisema Chintika
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Search This Blog