Home » » ASKOFU MKUU WA KANISA LA PENTECOSTE GOSPEL CHURCH AWATAKA WACHUNGAJI KUWA WAAMINIFU.

ASKOFU MKUU WA KANISA LA PENTECOSTE GOSPEL CHURCH AWATAKA WACHUNGAJI KUWA WAAMINIFU.

ASKOFU MKUU WA PGC AKIMIMINIWA MAFUTA TAYARI KWA KAZI YA BWANA.



ASKOFU MKUU WA PGC KULIA AKIWA NA ASKOFU MKUU WA EAST AFRIKA PAMOJA NA MAMA ASKOFU ALPHONCE NKANGA.






Baadhi ya wageni waalikwa wakishuhudia tukio likiendelea la kusimikwa kwa askofu NKHANGA


 Baadhi ya waumini wakimpongeza mama askofu mkuu wa kanisa la PGC Tanzania.



NA denis nyali iringa.

Askofu mkuu wa kanisa la PENTECOSTE GOSPEL CHURCH TANZANIA ALPHONCE KHANGA amewataka wachungaji kuwa waaminifu katika kazi ya MUNGU ili kuitenda kazi yake kwa ufasaha .
Akizungumza mara baada ya kusimikwa kuwa askofu mkuu wa Tanzania wa kanisa hilo amesema kwa sasa watumishi wengi wamekuwa si waaminifu katika kuitenda ya mungu hali inayopelekea wote kuonekana kuwa hivyo na kushindwa kuifanya kazi ya mungu.
                 
NKHANGA ameongeza kuwa si jambo la hekima kwa wachungaji kuandikwa na kuripotiwa na vyombo vya habari kwa kwa matendo ambayo hayambariki mungu bali waandikwe kwa kuihubiri injili na kuokoa roho za watu zilizopotea.
                   
Kwa upande wake askofu mkuu wa kanisa hilo afrika mashariki ZAKHARIA KALANJE amewasihii wachungaji kujiendeleza kimasomo ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya dunia kwa kuwa mungu si wa watu wapumbavu.

Tukio hilo la kusimikwa askofu mkuu wa Tanzania limefanyika katika ukumbi wa new life in Christ wilolesi na kuhudhuria na viongozi wa dini ,vyama na serikali.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Search This Blog