Home » » PAA ZA NYUMBA NNE ZAEZULIWA NA UPEPO IRINGA.

PAA ZA NYUMBA NNE ZAEZULIWA NA UPEPO IRINGA.





Upepo mkali uliombatana na mvua kiasi umeezua paa za nyumba nne na kuwaacha wakazi zaidi 15 wakiwa hawajui jambo la kufanya mara baada ya kukumbwa na kadhia hiyo.
Familia hizo ambazo zipo Mtaa wa Nduli, Kata ya Nduli, Manispaa ya Iringa zimekumbwa na kadhia hiyo hii leo majira ya saa kumi na moja kasoro jioni ambapo hata hivyo hakuna mtu alipepatwa na dhoruba ya kupata majeraha ama kifo baada ya janga hilo.





Akizungumzia tukio hilo mara baada ya kufika na kujionea hali halisi, Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Ndg Richard Kasesela ameuambia mtandao wa Wazo Huru kuwa, alipata taarifa hizo majira ya jioni ambapo aliamua kufika ili kujua ni kwa kiasi gani wakazi hao wamekumbwa na tatizo hilo.

Kasesela amesema ni tukio ambalo limemsikitisha kwa kiasi kikubwa kwani Mkoa huo bado upo katika maskitiko makubwa mara baada ya wakazi takribani 391 kutoka karibu kaya 99 kukumbwa na mafuriko katika Kijiji cha Kisinga, tarafa ya Pawaga yaliyosababisha serikali kutumia Helkopta kuwaokoa.

Kasesela amesema kuwa kesho asubuhi atatuma wataalamu kwa ajili ya kufanya tathimi ya kile kilichotokea ili kuona ni kwa namna gani serikali inaweza kusaidia wakazi hao ambao kwa sasa wamepatiwa hifadhi na majirani.

Kasesela amesema kuwa mvua zinazoendelea kunyesha Wilayani humo zimekuwa na changamoto kubwa kwa wakazi wa maeneo mbalimbali kutokana nakukosa makazi kwa sababu ya adha kubwa ambazo wamekuwa wakizipata, ambapo amesema serikali itajitahidi kukabiliana na kadhia yoyote itakayojitokeza ili kuwasaidia wananchi wanaokumbwa na matatizo yoyote.

Hata hivyo mkoa wa Iringa umeingia kwenye kadhia hii wakati zimepita siku chache tu mara baada ya vibanda 51 vya  wakulima wa mpunga kusombwa na maji katika vitongoji  vya Mboliboli na Kimande.

Aidha katika taarifa ya juzi iliyotolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Bi Amina  Masenza ilieleza kuwa serikali imefanya uchunguzi wa maji  katika mto Mlenge na katika  vyanzo vingine  vya maji kwenye tarafa ya Pawaga  ili  kuchunguza kama yana vimelea  vya Kipindupindu na kupitia  wataalam wa maji wa Bonde la Rufiji imebainika kwamba vyanzo vingi vya maji katika eneo hilo vina vimelea hivyo.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog