Home » » JAMANI DUNIA IMEKWISHA MTOTO WA MIAKA 7 ALAWITIWA NA WATU WAWILI KATIKA MTAA WA MTWIVILA MANISPAA YA IRINGA MWINGINE AVAMIA NYUMBA YA MWANAMKE NA KISHA KUMBAKA SOMA HAPA HABARI KAMILI.

JAMANI DUNIA IMEKWISHA MTOTO WA MIAKA 7 ALAWITIWA NA WATU WAWILI KATIKA MTAA WA MTWIVILA MANISPAA YA IRINGA MWINGINE AVAMIA NYUMBA YA MWANAMKE NA KISHA KUMBAKA SOMA HAPA HABARI KAMILI.



   IRINGA

Watu  wawili wanashikiliwa na jeshi la polisi  kwa kosa la kumlawiti mtoto wa miaka 7 mwanafunzi wa shule ya msingi umoja, mtwivila manispaa ya Iringa.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa Iringa ACP RAMADHANA ATHUMAN MUNGI amesema mtoto huyo amelawitiwa na watu wawili baada ya kumkamata na kumuingiza katika chumba na kwamba  Jeshi la polisi limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja anaefahamika kwa jina la JOHN LUCAS mwenye umri wa miaka 25.


Wakati huohuo kamanda Mungi amethibitisha kukamatwa kwa mtu mmoja ambaye ni mkazi wa kijiji cha mapogolo anaefahamika kwa jina la ADAM MBILINYI  kwa kosa la kuvunja nyumba ya mwanamke na kumbaka.


Kamanda Mungi amewataka watu wenye tabia za ulawiti na ubakaji kuacha tabia hizo kwa kuwa zinadhalilisha utu wa mtu na kwamba Jeshi la polisi halitawafumbia  macho wale wenye tabia hizo.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog