Home » » Kabla mabasi ya mwendokasi hayajaanza uyajue haya, ukifanya uzembe unalipa !!

Kabla mabasi ya mwendokasi hayajaanza uyajue haya, ukifanya uzembe unalipa !!


Mradi wa mabasi yaendayo kasi Dar es Salaam DART uko katika hatua za mwisho kukamilika na kuanza kutumika kama moja ya njia za kurahisisha usafiri katikati ya Jiji.
Mohamed Kuganda
Mohamed Kuganda, Kaimu Meneja Msimamizi wa Mradi wa DART.
Nimempata Kaimu Meneja msimamizi wa miundombinu mradi wa DART, Mohamed Kuganda… haya ni maneno yake ya kwanza kuhusu mradi huo >>> Kwa upande wa uharibifu wa miundombunu umekuwa ukitokea mara kwa mara na hauwezi kuzuilika ikiwemo madereva kugonga nguzo za taa za barabarani kutokana na kutumiwa wakati zikiwa katika ujenzi…”
DART II
Gharama za matengenezo ikitokea uharibifu huo zinamhusu nani >>> “Uharibifu ukitokea wakandarasi wanarekebisha kwa kuwa mradi uko chini yao lakini ikiwa tayari wamekabidhi, ni jukumu la TANROADS kufanya marekebisho“>>> Mohamed Kuganda.
Kwenye sentensi nyingine Mohamed Kuganda ana haya >>> “Ieleweke kwamba dereva akifanya uzembe kwa kugonga taa za barabarani ni wajibu wake kulipa na atashtakiwa kwa kosa la uharibifu wa mali za umma“.
DART III
Sehemu ya uharibifu kwenye barabara ya mwendokasi Dar.
Kuna suala la nauli pia mabasi ya mwendokasi yakianza safari, majibu yake ni haya >>> “Upande wa nauli mpaka sasa mchakato bado haujakamilika kwa kuwa ni mrefu na kwa sasa wadau wanafanya vikao kujadili, mchakato ukikamilika wananchi watafahamishwa“>>> Mohamed Kuganda.
Unaweza kutazama hii video hapa chini…
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog