Polisi Temeke Wakamata 'Panya Road' 18.

Jeshi la Polisi linawashikilia vijana zaidi ya 18 wenye umri kati ya miaka 14 na 20 kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya uhalifu katika maeneo ya Wilaya ya Temeke.

Kamanda  wa polisi wa Temeke, Gilles Muroto amesema leo kuwa vijana hao, wanaohusishwa na kundi la Panya Road linalofanya unyang'anyi maeneo ya jiji la Dar es Salaam, walikamatwa jana nyakati tofauti baada ya polisi kuendesha msako wa  kuzuia na kupambana na wahalifu.

Alisema vijana hao wanatoka maeneo ya Buza Kanisani, Chanika, Yombo Kirakala, Buza Changulu, Yombo Makangawe na moja anayeishi maeneo ya Mwananyamala lakini alikamatwa Temeke.

"Kama Kamanda Simon  Sirro alivyosema kuwa ni lazima wahalifu wadhibitiwe katika mko huu. Temeke hatuwez kumwangusha, tunatekeleza agizo lake," alisema Kamanda Muroto.

Alisema vijana hao wanajihusisha na vitendo vya uporaji wa mali mbalimbali kuanzia mitaani, pia kujeruhi watu hali inayosababisha wakazi wa eneo husika kuishi kwa hofu.

Alisema upelelezi ukikamilika watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani kwa hatua za kisheria.

Wakati huohuo, Kamanda Muroto amesema polisi inashikilia  mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 38, mkazi wa Buza baada ya kumkuta na puli 120 za dawa za kulevya aina ya bangi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi ya April 28 .

AINA ZA WASICHANA, TABIA ZAO KIMAUMBILE KATIKA MAPENZI



Inasemekana wadada wana tabia tofauti katika mapenzi kulingana na maumbo ya miili yao; karibu Mtembezini uelewe kwa kwa kina vitu vinavyoweza kukusaidia kutambua tabia za watu husika.

1.Wasichana wafupi wanaongoza kwa wivu wa mapenzi na kuwajali wapenzi wao

2. Wasichana warefu huwa hawawajali wapenzi wao na hawaogopi mahusiano kuvunjia hawajui kubembeleza hata kidogo.

3. Wasichana wenye DIMPOZ, MWANYA, MATEGE MBINUKO, MAHIPS NA KITEMBE, hawa huongoza kwa kutokuwa WAAMINIFU katika mapenzi.

4. Wasichana WANENE huongoza kwa kuwa na MAPENZI YA KWELI yaani akipenda amependa kisawasawa.

5. Wasichana WEMBAMBA hawa huwa ni WABISHI sana na hawa wanaongoza kwa kutendwa!

BLACK WOMANS6.Wasichana wenye NGOZI NYEUSI wanaongoza kwa KUTOA MIMBA na kupenda wanaume warefu na weupe.

7. Wasichana weupe wakiongoza kwa kuzalia nyumbani, na hawa weupe wengi wao huolewa wakiwa na watoto tayari huku wakipenda kuolewa na waarabu kuliko wanaume weusi.

Ripoti ya CAG Yawaweka Kikaangoni Vigogo wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD)

Ripoti iliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad imezichanganya Hospitali ya Taifa Muhimbili na Bohari ya Dawa (MSD), huku Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akihitaji maelezo ya kina kuhusu mkanganyiko huo. 
Ummy ameitaka MSD kuandika maelezo ya kina kwa maandishi, kuhusu vifaa vya Sh2 bilioni ambavyo viko njiani kwenda Muhimbili kwa miaka minne sasa, kabla wizara yake haijatoa tamko rasmi. 
Mkurugenzi wa MSD, Laurean Bwanakunu  jana alisema bohari haina mzigo wowote ulio njiani kuelekea Muhimbili bali imekuwa ikisambaza dawa zake nchi nzima. 
Bwanakunu alisema tatizo lililojitokeza ni mfumo wa kompyuta ambao unaonyesha mzigo upo njiani, hivyo muamala katika kompyuta unavyoshindwa kukamilika, mzigo lazima uonekane upo njiani. 
“Mwaka 2012 tulibadilisha mfumo wa kompyuta kutoka wa awali mpaka tunaotumia sasa, hivyo kuna miamala ilihitaji kubadilishwa, mwaka huu tulifanya zoezi la kukamilisha baadhi na si kwa Muhimbili pekee kwa mfano kuna mzigo unatoka MSD Ubungo kwenda Muleba ukifika kule mtu anashindwa kuingiza kwenye mfumo kwamba umepokelewa,”alisema Bwanakunu. 
Alifafanua kwamba majibu ya MSD kwa CAG yalieleza kuwa walitengeneza timu ya uchunguzi na baadhi ya watu walichukuliwa hatua, “nimeshachukua hatua za haraka baada ya kupata hiyo ripoti, tangu mwanzoni mwa mwaka huu wale ambao hawakujaza hiyo miamala tulishawachukulia hatua, hakuna mali iliyopotea MSD.” 

Taarifa zaidi zinaeleza kwamba kuna ripoti ya Muhimbili ambayo inaonyesha katika vitabu kwamba kuna mzigo ambao Muhimbili iliununua kutoka MSD, lakini haujafika, lakini Bwanakunu alipoulizwa alisema hakuna vitabu vinavyoonyesha kuwa Muhimbili inadai vifaa tiba na dawa MSD. 
Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru alisema kwa taarifa alizonazo mpaka sasa CAG alifanya ukaguzi katika vitabu vya MSD na si wao na alipouliza vifaa viko wapi alijibiwa kuwa vinakwenda MNH. 
Alisema kuwa Watanzania wawe na subira na kwamba watapewa majibu kesho (leo), baada ya Muhimbili kupekua kwa kina vitabu vya mwaka 2012, ili kujiridhisha iwapo vifaa vilipokelewa au havikuwahi kununuliwa Muhimbili. 
“Hiyo ripoti tumeiona leo Jumanne. Hayo mambo yametokea mwaka 2012 huwezi kuwa na jibu la kila kitu, kesho tunataka tukapitie hiyo ripoti kwa sababu ni ukaguzi wa MSD, tukaangalie vitabu hivyo vifaa vilifika?”Alisema Museru. 
Naye Waziri Ummy Mwalimu alisema katika ripoti hiyo kuna hoja mbili ambazo ni MSD na TFDA, huku akifafanua kwamba amezungumza na Mkurugenzi wa MSD lakini hajaridhika na majibu na kumtaka aandike maelezo ya kina. 
“Nimetaka maelezo ya maandishi kutoka kwa MSD na TFDA kuhusu ripoti ya CAG tumekubaliana na Katibu Mkuu walete maandishi ndiyo tutatoa msimamo rasmi wa wizara, kwa upande wa MSD ndiyo maana tuliweka pembeni wale wakurugenzi wanne sababu ya changamoto hii ambayo CAG amekutana nayo,” alisema Ummy

Rais Magufuli Asamehe Wafungwa 3,551

Rais John Magufuli ametoa msamaha kwa wafungwa 3,551, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 52 ya Muungano wa Tanzania.

Taarifa iliyotolewa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Meja Jenerali Projest Rwegasira ilisema wafungwa 580 wataachiwa huru, huku wengine 2,971 watapunguziwa moja ya sita ya vifungo vyao.

Alisema rais ametoa msamaha huo kwa kutumia madaraka aliyopewa chini ya ibara ya 45(1)(d) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aliwataja watakaonufaika na msamaha huo kuwa ni wafungwa wenye ugonjwa wa ukimwi, kifua kikuu na saratani ambao wapo kwenye hatua za mwisho. Wengine ni wazee wenye umri wa miaka 70 na kuendelea, wajawazito na wale waliongia na watoto gerezani.

Wafungwa wengine watakaonufaika na msamaha huo ni wenye ulemavu wa akili ambao wamethibishwa na jopo la waganga kuwa wana tatizo hilo.

Katibu mkuu wa wizara hiyo alisema msamaha huo hautawagusa wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kunyongwa au kifungo cha maisha jela.

Pia, wafungwa wanaotumikia kifungo kwa makosa ya usafirishaji na matumizi ya dawa za kulevya, upokeaji na utoaji rushwa, matumizi mabaya ya madaraka, unyang’anyi kwa kutumia silaha na kubaka ni miongoni mwa waliokosa msamaha huo.

Wengine ambao hawataguswa na msamaha huo ni wale wanaotumikia vifungo kwa makosa ya kupatikana na  silaha, wizi wa magari na pikipiki, kuwapa mimba wanafunzi na ubadhirifu wa fedha za Serikali.

Wafungwa wengine watakaoendelea kubaki magerezani ni wale waliohukumiwa kutokana na usafirishaji wa nyara za Serikali na ujangili, utekaji wa watoto, biashara ya binadamu, kukutwa na viungo vya binadamu na waliojaribu kutoroka wakiwa chini ya ulinzi.

Katika maadhimisho ya Uhuru yaliyofanyika Desemba 9, 2015, Rais Magufuli aliwasamehe wafungwa 2,336, kati ya hao 117 waliachiwa huru huku 2,219 wakipunguziwa moja ya sita ya vifungo vyao.

Kwa idadi hiyo mpaka sasa wafungwa 5,887 wamenufaika na msamaha wa Rais Magufuli tangu aingie madarakani baada ya kushinda katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, 2015.

Mwenyekiti Aweka Majina HEWA Mradi wa Kuokoa kaya Masikini (TASAF )

Wananchi wamemkataa mwenyekiti wa kitongoji cha Mwanogi kijiji cha Bulima, Kata ya Nyashimo wilayani Busega katika Mkoa wa Simiyu, wakimtuhumu kuweka majina hewa katika mradi wa kuokoa kaya masikini unaosimamiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf).

Mwenyekiti huyo wa kitongoji, Ester Ng’ombe anatuhumiwa pia kufanya kazi kwa ubaguzi wa vyama vya siasa.

Akizungumza katika kikao, mwenyekiti wa kamati ya mipango na fedha ya kijiji cha Bulima, Zablon Ntinika alisema wamefikia uamuzi wa kumsimamisha kazi mwenyekiti huyo baada ya uchunguzi walioufanya kubaini majina matano ambayo ni hewa yakipatiwa fedha.

Alisema wamekuwa wakifuatilia kwa karibu mwenendo wa mwenyekiti huyo katika utendaji wake wa kazi katika kitongoji hicho lakini wamebaini mengi. 
Mwenyekiti huyo anayetuhumiwa, alipoulizwa kuhusu madai hayo, alisema kuwa yeye hayatambui bali ni siasa za chuki dhidi yake.

Ng’ombe alisema chanzo si majina feki bali ni siasa zinazochochewa na wanasiasa wa kata hiyo ambao wanataka kuichafua sifa yake ili aweze kuondolewa na wananchi waliomchagua.

Mwanafunzi Amkaanga kortini polisi anayedaiwa kumbaka katika kibanda cha ulinzi cha benki.

Mwanafunzi wa kidato cha tatu, juzi alimkaanga askari polisi anayedaiwa kumbaka kwa kuieleza Mahakama jinsi alivyotendewa kitendo hicho katika kibanda cha ulinzi cha benki.

Akitoa ushahidi mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya Misungwi, Ruth Mkisi, shahidi huyo alidai siku ya tukio askari huyo, Raphael Sixstus (30), alimuita alipokuwa akipita karibu na Benki ya CRDB Tawi la Misungwi, alipoitikia wito ghafla alivutiwa ndani ya kibanda hicho na kumbaka.

“Wakati akinitendea kitendo hicho, alikuwa akinitishia kisu huku akiniambia nikipiga kelele ataniua, niliogopa nikaa kimya ingawa niliumia na kutokwa damu nyingi sana,” alidai shahidi huyo.

Akiongozwa na Mwendasha Mashtaka wa Polisi, Doreth Mgenyi, mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 16 alidai kabla ya kumbaka, mshtakiwa huyo alimvua nguo zote za ndani.

Awali, Mwendesha mashtaka alipokuwa akimsomea makosa mshtakiwa huyo alidai kuwa Novemba 20, mwaka jana, akiwa eneo la lindo katika Benki ya CRBD Tawi la Misungwi, alimbaka mwanafunzi huyo saa 1.00 usiku wakati akitoka mashine kusaga unga katika maeneo ya Bomani.

Hakimu Mkisi aliahirisha kesi hiyo hadi leo itakapoendelea kusikilizwa kwa upande wa mashtaka kuita mashahidi wengine. Mshtakiwa yuko nje kwa dhamana.

Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo April 27 2016 kwenye, Udaku, Hardnews na michezo


20160427_053542
20160427_043807
20160427_043852
20160427_043905
20160427_053622
20160427_053635
20160427_043914
20160427_043929
20160427_043939
20160427_044001
20160427_044011
20160427_044020
20160427_044030
20160427_044044
20160427_044055
20160427_044106
20160427_044117
20160427_044135
20160427_044145
20160427_044158
20160427_044206
20160427_044225
20160427_053650
20160427_053700
20160427_053759

AGIZO LA MAKONDA ,Polisi Dar Yakamata Ombaomba 45 Dar, 17 Wapelekwa gerezani

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro alisema jana kuwa jeshi hilo kwa kushirikiana na Idara ya Ustawi wa Jamii, wanafanya utaratibu wa kuhakikisha watu hao wanarudishwa mikoani walikotoka. 
 
“Kazi hii inaenda vizuri na ombaomba wachache wamebakia ambao wakiwaona askari wanakimbia na kutokomea kusikojulikana,”alisema Sirro. 
Katika tukio lingine, Polisi wanawashikilia watuhumiwa 96 wenye umri wa miaka 15-18 wanaodaiwa kujihusisha na matukio ya kuvamia nyumba na kuiba usiku. 
 
Kamanda Sirro alisema watuhumiwa hao wanajulikana kwa jina maarufu la ‘kumi ndani kumi nje’, walikamatwa katika maeneo mbalimbali ya jiji na wanaendelea kuhojiwa na polisi, upelelezi utakapo kamilika watafikishwa mahakamani. 
 
“Watuhumiwa hawa wanavunja milango kwa mawe makubwa na kuiba televisheni na simu, upelelezi unaendelea na wanaendelea kutajana hivyo tutawakamata na wengine,” alidai kamanda huyo. 
 
Wakati huohuo, Kamanda Sirro alisema makosa ya kuvunja Sheria ya Usalama Barabarani mkoani hapa, yameliingizia jeshi hilo mapato ya Sh463 milioni kwa muda wa siku 10. 
 
“Jeshi la Polisi kazi yetu ni kusimamia sheria siyo kukusanya mapato, hivyo watu wazingatie sheria,” alisema kamanda huyo. 
 
Alisema ili kupunguza matukio ya uhalifu, jamii haina budi kuhakikisha kunakuwa na vikundi vya ulinzi shirikishi katika mitaa yao na Serikali za Mitaa zinapaswa kuhakikisha jambo hilo linazingatiwa na linafanyika.

Mchina Ahukumiwa Miaka Mitatu Jela Kwa Kuuza Bidhaa Bila Kutoa Risiti

Mahakama ya Wilaya ya Ilala imemhukumu kifungo cha miaka mitatu jela au kulipa faini ya Sh4.5 milioni, mfanyabiashara Huifang Ma baada ya kupatikana na hatia ya kuuza bidhaa na kushindwa kutoa risiti kwa kutumia mashine ya kieletroniki. 
 
Ma ambaye ni raia wa China na mkazi wa Mtaa wa Narung’ombe eneo la Kariakoo, alihukumiwa kifungo hicho baada ya kukiri mashtaka mawili yaliyokuwa yakimkabili likiwamo la kushindwa kujisajili kulipa kodi ya ongezeko la thamani (Vat). 
 
Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mwanadamizi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Said Mkasiwa alisema kwa kuwa mshtakiwa alikiri mashtaka yanayomkabili, anatakiwa kulipa faini au kwenda jela miaka mitatu. Hata hivyo, Ma alilipa faini na kuachiwa huru. 
 
Katika hati ya mashtaka, ilidaiwa kuwa Machi 23, mwaka huu eneo la Karikaoo, mshtakiwa alishindwa kutoa risiti za kieletroniki kwa mteja wake. 
 
Ilidaiwa kuwa siku hiyo mshtakiwa ambaye ni mmiliki wa Kampuni ya HM Textile Co Ltd iliyopo Mtaa wa Agrey, Kariakoo, alishindwa kutumia mashine za EFDs kwa ajili ya kutoa risiti kwa wateja walionunua bidhaa dukani kwake.
 
Kosa la pili, mshtakiwa alishindwa kujisajili kama mlipa kodi wakati akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Wafanyakazi wa TMA watakiwa kutumia mfumo wa kisasa kuhifadhi taarifa muhimu za ofisi

Watumishi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, (TMA) wametakiwa kuachana na mfumo wa zamani wa kutumia makaratasi katika kuhifadhi taarifa zao muhimu na badala yake kuanza  kutumia mfumo wa kisasa wa kieletroniki.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Pof. Makame Mbarawa  jana jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano na wafanyakazi hao na kueleza kuwa kwa kufanya hivyo kutasaidia kupunguza matumizi ya fedha za kununulia  karatasi.

“Katika ofisi zenu nimeona kila mtu anakomputa ni jambo zuri hivyo zitumieni katika kuhifadhi taarifa muhimu za taasisi yenu kwa mfumo wa kieletroniki” alisema Mhe.Prof.Mbarawa.

 Aliongeza kwa kusema kuwa serikali imetumia fedha nyingi katika kujenga mkongo wa taifa wa kuhifadhi taarifa muhimu  hususani za serikali pamoja na Taasisi zake hivyo ni budi  waanze kuutumia mkongo huo kwa kuhifadhia taarifa zao.

Pia aliongeza kwa kuwataka watumishi kuwa waadilifu,wachapaka kazi ,wabunifu na kuwa na uwazi baina ya watendaji wa juu na watumishi wa ngazi ya chini kwa kushirikiana na  wafanyakazi wa mikoani .

“Watanzania wanamatarajio mengi kutoka kwetu  katika kukuza uchumi wa nchi hivyo ni wajibu wetu kutimiza matarajio yao kwa kuwapatia mahitaji muhimu ikiwemo miundo mbinu imara ya barabara, bandari ,shirika la ndege la kisasa na utabiri  wa hali ya hewa wenye uhakika ” alisema Mhe.Prof.Mbarawa.

Prof.Mbarawa  alitoa wito kwa kuwataka  watumishi hao kufanya kazi kwa ushirikiano  kila mmmoja kujituma katika eneo lake la kazi ili kuleta matokeo yaliyobora na hivyo kukuza uchumi wa nchi kwa kufikia uchumi wa kati.

Ripoti ya CAG Yaanika 'Madudu' Kibao Serikalini

Wakati Rais John Magufuli akipambana dhidi ya ufisadi, uzembe na ukwepaji kodi na uovu mwingine dhidi ya mali za umma, ripoti mpya ya ukaguzi iliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali inaonyesha ana kazi kubwa zaidi kupata ushindi kwenye vita hiyo. 

Ripoti hiyo ya mwaka 2014/ 2015 iliyowasilishwa bungeni jana na CAG Mussa Juma Assad imeibua uozo zaidi kwenye halmashauri, taasisi za Serikali na mashirika ya umma, ikibainisha kuwa nchi ina tatizo kubwa zaidi ya watu ambao wamekuwa wakishughulikiwa na Serikali ya Awamu ya Tano. 
 
Ripoti hiyo ya pili ya Professa Assad tangu ateuliwe kushika nafasi hiyo mwaka juzi, imegusa taasisi zilizowahi kuwa chini ya Rais John Magufuli na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako na Balozi Asha Rose Migiro, ambaye alikuwa Waziri wa Sheria na Katiba. 
 
Ripoti hiyo pia inaonyesha ufisadi katika ununuzi na uingiaji mikataba uliofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), matumizi yasiyo ya lazima kwenye Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Afya, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jeshi la Wananchi, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi na mkoa wa Tabora. 
 
Pia ripoti hiyo imebainisha kuwa mapendekezo mengi ambayo CAG amekuwa akiyatoa kwa takribani miaka saba sasa, hayatekelezwi. 
 
Katika ripoti hiyo, CAG anaonyesha dosari kwenye utendaji wa Wakala wa Huduma za Ufundi na Umeme (Temesa), na Wakala wa Barabara (Tanroads), taasisi zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi ambayo wakati huo ilikuwa ikioongozwa na Dk Magufuli. 
 
Profesa Ndalichako alikuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), wakati NEC imeguswa na ripoti hiyo katika suala la mchakato wa kuandika Katiba upya ulioongozwa na Wizara ya Katiba na Sheria. 
 
Ripoti hiyo ya Profesa Assad pia imebainisha kuwa Deni la Taifa, ambalo hutokana na fedha zinazopowa kutoka ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kugharimia matumizi ya Serikali, limekuwa kwa tofauti ya Sh7 trilioni. 
 
Tangu aingie madarakani Novemba 5 mwaka jana, Dk Magufuli amekuwa akitumia ripoti zilizopita za CAG kusimamisha kazi au kutengua uteuzi wa watumishi wa umma wanaotuhumiwa kujihusisha na ufisadi, lakini amekuwa akikosolewa kuwa hajaweka mfumo wa kukabiliana na hali hiyo. 
 
Katika ripoti hiyo, CAG anasema Temesa ilinunua kivuko chenye kasi ndogo kuliko ilivyotarajiwa na hadi ulipokuwa unafanyika ukaguzi Agosti 2015, chombo hicho kilikuwa hakifanyi kazi kwa zaidi ya mwaka. 
 
“Kuhusu dosari katika ununuzi wa kivuko chenye thamani ya Sh7,916,955,000, Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Umeme, mitambo na ufundi (Temesa) iliingia mkatabana M/s Johs.Gram-Hanssen Bergensgade 10, DK 2100 Copenhagen Oe Denmark wa ununuzi wa kivuko cha Dar es Salaam –Bagamoyo chenye thamani ya Dola za Marekani 4,980,000 bila Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT),” anasema CAG. 
 
“Dosari zifuatazo zilibainika katika manunuzi hayo. Kasi ya kivuko haikuzingatia matakwa ya mnunuzi.  Ripoti ya mtaalamu wa ukaguzi ilibainisha kwamba kiwango cha juu na chini cha kasi ya kivuko wakati wa majaribio kilikuwa na kiwango kati ya knots 19.45 na knots 17.25 kinyume na makubaliano yaliyoainishwa kwenye mkataba wa kasi ya kiwango cha 20,” anafafanua.
 
“Pili kivuko kilikabidhiwa bila hati ya makabidhiano Novemba 17, 2014 baada ya ucheleweshwaji wa siku 16; Pia nilibaini kwamba mpaka wakati wa ukaguzi, Agosti 2015, hati ya makabidhiano ilikuwa haijatolewa na mzabuni.” 
Ununuzi wa feri hiyo uliwahi kuzua sakata bungeni huku wabunge wa upinzani wakilalamika kwamba kilikuwa bomu kwani kinatumia zaidi ya saa tatu kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo badala ya dakika 45 za gari. 
 
Eneo jingine lililoguswa na CAG ni la malipo yaliyofanywa na Tanroads kwa makandarasi waliomaliza kazi zao. Kwamba moja ya matatizo makubwa ya taasisi hiyo ni udhaifu katika menejimenti. 
 
“Wakala wa Barabara (Tanroads) iliingia mikataba mbalimbali ya ujenzi wa barabara na madaraja. 
 
"Wakati wa ukaguzi nilibaini kwamba baadhi ya mikataba haikukamilika kwa muda uliopangwa kutokana na kuchelewa kwa ulipaji wa fedha. 
  
"Pia, nilibaini kwamba ucheleweshwajiwa malipo ya kati ya mikataba 16 ulisababisha ulipaji wa riba kiasi cha Sh 5,616,652,022 na Dola za Marekani 686,174.86,” alisisitiza CAG. 
 
Profesa Assad amezungumzia pia ukaguzi maalumu alioufanya kuhakiki fedha zilizowahi kutolewa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa taasisi mbalimbali zilizoko chini yake. 
 
Ukaguzi huo ulifanywa kutokana na ombi lililowasilishwa na katibu wa Bunge kwa barua yenye Kumb. NaCBC.155/188/01/26 ya Desemba 19, 2013. 

Bunge lilitaka kujua kama fedha zilizotolewa na wizara hiyo kwenda idara na taasisi zilizo chini yake zilipokewa na kutumiwa na wahusika kama ilivyopangwa. 
 
Katika ukaguzi huo, CAG alibaini kasoro katika vitabu vya akaunti za fedha vya Necta mwaka 2010, Sekretarieti ya Elimu ya Jumuiya ya Madola, Chuo Kikuu Huria (OUT), na Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (Adem). 
 
“Udanganyifu wa malipo ya Sh185,350,000 yaliyolipwa Necta. Aprili 2010 kiasi cha 185,350,000 kilitumwa Necta kama matumizi ya kawaida. Wakati wa ukaguzi ilibainika kuwa kiasi hiki cha fedha hakikuandikwa kwenye vitabu vya uhasibu vya Necta. Hata hivyo, ilibainika kuwa stakabadhi ya mapokezi ya fedha hizo iliyotolewa na watumishi wasio waaminifu wa Necta ilikuwa ya kugushi,” anasema. 
 
“Kuhusu fedha zilizopelekwa OUT ni kwamba kati ya mwaka 2009/2010 Wizara ilihamisha Sh90,000,000 kwenda Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola, ni kiasi cha Sh40,734,000 ambacho kilipokewa huku Sh49,266,000 hakijulikani. 
 
“Pia katika mwaka wa fedha 2010/2011 Wizara ilipeleka OUT Sh10,486,252,913 lakini ni Sh10,427,109,020 tu zinazoonekana kwenye vitabu huku Sh59,143,893 zikiwa hazimo kwenye vitabu.” 

Vilevile, CAG amesema katika ukaguzi huo Sh188, 838,528 zilizopelekwa Adem mwaka 2009/2010 zimeyeyuka. Mwaka huo Wizara ilipeleka Sh712,798,788 kwa taasisi hiyo, lakini vitabu vinaonyesha Sh523,960,260 zilipokewa na kurekodiwa, huku Sh188, 838,528 zikikosekana kwenye vitabu. 
 
Mbali ya CAG kuonyesha madudu katika matumizi ya fedha, pia ameonyesha matumizi mabaya ya Sh7,080 milioni katika mchakato wa uchapaji Katiba Inayopendekezwa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya April 26 .

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog