Aliyekuwa
mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM, Frederick Mwakalebela amefungua kesi
ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Ubunge wa jimbo la Iringa mjini
yaliyompa ushindi Mchungaji Peter Msigwa wa Chadema huku akiitaja kofia
ya M4C katika shtaka lake.
Msajili
msaidizi wa mahakama kuu ya kanda ya Iringa , Ruth Massama amesema kuwa
Mwakalebela alifungua shtaka hilo mahakamani hapo Oktoba 30 mwaka huu.
Katika
shitaka hilo, pamoja na mambo mengine, Mwakalebela anamtuhumu Msigwa
kwa kuvunja sheria ya uchaguzi kwa kuvaa kofia yenye nembo ya M4C
inayotumiwa na Chadema, katika siku ya kupiga kura.
Kadhalika,
mlalamikaji huyo anamtuhumu mwangalizi wa uchaguzi kwa kukiuka sheria
na kanuni za uchaguzi wakati wa zoezi la kupiga na kuhesabu kura.


0 comments:
Post a Comment