Novemba 9, 2015 kulikuwa na headlines
kwenye mitandao mbalimbali kuhusiana na video ikionesha Askari wa
usalama wa barabarani anayefahamika kwa jina la Anthony Temu kutoka kituo cha polisi kinachojulikana kama Kabutu huko Tanga akijihusisha katika tendo la rushwa.
Sasa taarifa iliyonifikia ni kwamba
askari huyo aliyeonekana katika mitandao jana akipokea rushwa Kabuku,
Tanga amefukuzwa kazi na kukabidhiwa kwa TAKUKURU kwa mashitaka ya Rushwa.
Unaweza ukabonyeza play kumsikiliza
kamanda wa polisi mkoani Tanga, Zuberi Mwombeji akizungumza kuhusiana na
askari huyo kukamata na kukabidhiwa kwa TAKUKURU.


0 comments:
Post a Comment