Zaidi ya Watu 900 Wadaiwa Kupoteza Maisha kwa Tetemeko la Ardhi Nchini Nepal
TETEMEKO
la ardhi limetokea nchini Nepal jana na na kupoteza
maisha ya watu ya 900 na kuangusha Mnara wa Karne ya 19 Mjini,
Kathmandu pamoja na kusababisha maporomoko ya theluji kutoka katika
milima.
Taarifa
zinadai kuna uharibifu katika maeneo ya nje ya kitovu cha tetemeko hilo
lenye ukubwa wa kipimo cha richter cha 7.9 maili 50 kutoka Pokhara mji
wa pili kwa ukubwa nchini Nepal.
Tetetemeko
hilo la ardhi ni kubwa kabisa kuwahi kuikumba nchi hiyo katika kipindi
cha miaka 81 na pia limesababisha athari katika majimbo ya nchi jirani
kaskazini mwa India na Bangladesh.
Kunauwezekano vifo hivyo vinaweza kuongezeka katika Bonde la Kathmandu ambalo lina watu milioni 2.5.
Naibu
balozi wa Nepal mjini New Delhi Prasad Pandey amesema inahofiwa kuwa
mamia ya watu wamekufa na kuna ripoti ya kuwepo kwa uharibifu mkubwa
kila sehemu kubwa na kwamba sio tu katika baadhi ya maeneo ya Nepal bali
ni nchi nzima imeathirika.
Nepal
ilikumbwa na tetemeko kubwa la ardhi kuwahi kurekodiwa nchini humo hapo
mwaka 1934 likiwa na kipimo cha 8.0 ambapo watu 8,500 walipoteza maisha
yao.

Baadhi
ya Waokoaji wakiwa wamsaidia mmoja wa waathirika wa Tetemoko hilo
aliekuwa amefukiwa kwenye kifusi ya moja ya majembo yaliyoporokoma
kutokana na tetemeoko hilo.

Sehemu ya athari za tetemeko hilo.

Jitihada za kuokoa waliofunikwa na kifusi zikiendelea.

Wananchi wa Nepal wakishirikiana kwa pamoja kuvuta kamba.

Ramani inayoonyesha sehemu iliyokumbwa na tetemeko hilo.
0 comments:
Post a Comment