Home » »

                              Hapa wakati alipokuja Tanzania kwenye tamasha la pasaka
 
                     Malope kuja na albamu mpya ya nyimbo za kiingereza pamoja na za tenzi
Malkia wa muziki wa gospel barani Afrika bi Rebecca Malope ameweka bayana kwamba yupo kwenye mchakato wa kurekodi album maalum ambayo itakuwa ya nyimbo za kiingereza pekee, ambapo mpaka sasa kupitia kampuni yake ya muziki mchakato wa kuandaa album hiyo tayari umeanza.

Mwimbaji huyo aliyepata mafanikio makubwa katika tasnia ya muziki wa gospel tayari ana album 33 za audio ikiwemo mpya aliyorekodi mapema mwezi wa pili mwaka huu akiwashirikisha Tshwane Gospel Choir, ambayo kwa upande wa DVD itakuwa ya 5 lakini ya kwanza kurekodiwa live. Rebecca ameweka wazi mpango wake huo wakurekodi album maalumu ya nyimbo za kiingereza wakati akihojiwa kupitia kipindi cha runinga cha Expresso kinachorushwa na Sbc3.

Mwimbaji huyo pia ameweka bayana kwamba anatarajia kutoa kitabu cha nyimbo zake za tenzi( ama album) kwa lugha mbalimbali nakuwataka mashabiki wake na wapenzi wa gospel kwa ujumla kukaa mkao wa kupokea album hiyo pamoja na kitabu.Rebecca amekuwa akitoa nyimbo kwa lugha ya nyumbani kwao lakini pia amekuwa mda mwingine akiweka wimbo mmoja wa kiingereza katika album zake, hata hivyo hakuweka bayana kama nyimbo katika album hiyo itakuwa mpya tupu ama atachanganya na za zamani.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Search This Blog